Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM TAIFA (Njombe)
ambaye pia ni Afisa kutoka UVCCM Makao Makuu Ndugu Omega Thobias amekuwa Mgeni
Rasmi kwenye mahafali ya Kidato cha Nne Shule ya Sekondari Migombani iliyopo
Tabata Segerea Jijini Dar Es Salaam.
Ndg Omega Thobias akiiwakilisha UVCCM
kupitia Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi UVCCM TAIFA Ndg Hassan
Bomboko amewaasa wanafunzi wanaohitimu kuwa raia wema pindi watakapomaliza
mitihani yao na ili kuondokana na vitendo viovu mitaani amewaomba Wazazi,
Walezi, Ndugu, Jamaa na marafiki wa wanafunzi kuendelea kuwasimamia kwa
kuwaendeleza kielimu hasa kuwapeleka Vyuo vya VETA ili wapate Ujuzi utakao
wasaidia maishani mwao.
"Ujana wetu tusiutumie vibaya kwa
kujiona sisi ndio wasomi kuliko wengine, Tuweni wanyenyekevu na wenye uchaji wa
kujifunza mambo mbalimbali yenye tija ili tuweze kuisaidia serikali yetu
inayoongozwa na Rais wetu Dkt John Pombe Magufuli inayotekeleza Ilani ya Chama
cha Mapinduzi ya Uchaguzi wa mwaka 2015/2020 hasa katika sera ya Tanzania ya
Viwanda" amesema Ndg Omega Thobias.
Ndg Thobias amewajuza wanafunzi hao
umuhimu wa kuwa na ujuzi na kusema kwamba Ujuzi haufi wala kupotea, hivyo
msiishie kusoma tu darasani ili mfaulu mitihani ni vema kila akaona kitu
akipendacho na anachokimudu akaendelea kujifunza kwa muda wake wa ziada iwe ni
kusuka nywele, ushonaji, uhunzi, ufundi umeme, upambaji, uchoraji, na sanaa
yote kwa ujumla.
Awali, Mgeni Rasmi alipata nafasi ya
kuonyeshwa Majaribio ya Kisayansi (*Experiments) kwenye *Maabara Shuleni hapo
ambapo wanafunzi wa Kidato cha Nne wanaohitimu na wale wa Kidato cha tatu na
cha kwanza walifanya vizuri kwa vitendo.
Aidha, Wanafunzi wa Sekondari ya Migombani
walionyesha uwezo wao kupitia vipaji kwa uigizaji, ushairi, muziki wa kizazi
kipya, ngoma na uigaji sauti ambapo Mgeni Rasmi aliwasisitiza kuvithamini
vipawa walivyonavyo na kuviendeleza ili kuja kunufaika navyo kwani Kipaji ni
Mtaji.
Naye, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya
Migombani Mwl Mama Chalamila ameusifu Utendaji wa Rais Dkt Magufuli na Waziri
wa Elimu Profesa Ndalichako na Uongozi wa Umoja wa Vijana wa Chama cha
Mapinduzi (UVCCM) kwa jinsi ulivyo karibu na Taasisi za kiraia na
kiserikali na kwa kipekee UVCCM kukubali mwaliko wao kwenye mahafali
hiyo.
0 comments:
Post a Comment