Tume ya Madini iliundwa kwa mujibu wa kifungu cha 21
cha Sheria ya Marekebisho Anuwai ya Sheria ya Madini Na. 7 ya Mwaka 2017. Mnamo
tarehe 17 Aprili, 2018, Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dr. John
Pombe Joseph Magufuli, kulingana na Sheria tajwa, aliteua Mwenyekiti na Makamishna
wa Tume ya Madini. Ili kutekeleza majukumu yake, Tume ilifanya kikao chake cha
kwanza tarehe 30 Aprili, 2018 Jijini Dodoma. Pamoja na mambo mengine, Tume
iliazimia mambo yafuatayo:
i.
Ofisi za Makao
Makuu ya Tume ya Madini zitakuwa Jijini Dodoma katika Ofisi za Wizara ya Madini;
ii.
Kuimarisha
usimamizi wa Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 na marekebisho yake ya Mwaka 2017
kwa lengo la kuhakikisha kuwa Serikali inamiliki hisa zisizopungua asilimia 16 ya
mtaji wa Kampuni zinazomiliki migodi ya kati (MLs) na mikubwa (SMLs), Wazawa
wanashirikishwa ipasavyo katika Miradi ya Madini na kunufaisha jamii katika
maeneo ya migodi na Taifa kwa ujumla;
iii.
Kuwajulisha
wamiliki wote wa leseni zote za kuhodhi maeneo (Retention Licences – Jedwali Na. 1) kuwa leseni zao zimefutwa kwa
mujibu wa Sheria ya Madini ya Mwaka 2010 ikisomwa pamoja na marekebisho yake ya
mwaka 2017 na Kanuni ya 21 ya Kanuni za Madini (Haki Madini), 2018 Tangazo la
Serikali Na.1/2018 na kwamba maeneo ya leseni hizo yamerudishwa Serikalini bila
hakikisho la kupewa tena;
Jedwali Na. 1: Orodha ya
leseni za kuhodhi maeneo zilizofutwa
Namba ya Leseni
|
Jina la Mmiliki
|
Aina ya Madini
|
Tarehe ya kutolewa
|
Tarehe ya kuisha muda
|
Ukubwa (Km2)
|
Mkoa/Wilaya
|
Hali halisi
|
RL 0001/2009
|
Kabanga Nickel Company Limited
|
Nickel
|
02/05/2009
|
01/05/2019
|
201.85
|
Kagera/ Ngara
|
Imefutwa
|
RL 0006/2009
|
National Mineral Development
Corporation Limited
|
Gold
|
31/12/2009
|
30/12/2019
|
21.27
|
Shinyanga/ Kahama
|
Imefutwa
|
RL 0009/2014
|
Bafex Tanzania Limited
|
Silver, gold & Copper
|
01/09/2014
|
31/08/2019
|
12.58
|
Mbeya/ Chunya
|
Imefutwa
|
RL 0010/2014
|
Bafex Tanzania Limited
|
Silver, gold & Copper
|
01/09/2014
|
31/08/2019
|
12.59
|
Mbeya/ Chunya
|
Imefutwa
|
RL 0011/2014
|
Bafex Tanzania Limited
|
Silver, gold & Copper
|
01/09/2014
|
31/08/2019
|
11.83
|
Mbeya/ Chunya
|
Imefutwa
|
RL 0012/2014
|
Bafex Tanzania Limited
|
Silver, gold & Copper
|
24/09/2014
|
23/09/2019
|
11.27
|
Mbeya/ Chunya
|
Imefutwa
|
RL 0014/2014
|
Mabangu Mining Limited
|
Gold
|
31/10/2014
|
30/10/2019
|
2.94
|
Geita/Mbogwe
|
Imefutwa
|
RL 0015/2014
|
Resolute (Tanzania) Limited
|
Gold
|
31/10/2014
|
30/10/2019
|
0.91
|
Geita/Mbogwe
|
Imefutwa
|
RL 0016/2015
|
Wigu Hill Mining Company Limited
|
Rare Earth Elements
|
13/02/2015
|
12/02/2020
|
15.14
|
Morogoro
|
Imefutwa
|
RL 0017/2015
|
Nachingwea Nickel Limited
|
Nickel
|
21/04/2015
|
20/04/2020
|
48.8
|
Lindi /Nachingwea
|
Imefutwa
|
RL 0013/2014
|
Precious Metals Refinery Company
Limited
|
Nickel
|
10/10/2014
|
09/10/2019
|
25.7
|
Simiyu/ Bariadi & Busega
|
Imefutwa
|
iv.
Hadi kufikia
tarehe 04/07/2017, kulikuwa na jumla ya maombi mapya ya leseni za uchimbaji wa
kati (MLs) zipatazo 15 na ya kuhuisha 21. Pia maombi ya leseni za uchimbaji
mdogo wa madini (PMLs) yalikuwa 4,345 katika Ofisi za Madini za Mikoa na Wilaya
kote nchini. Kadhalika, hadi kufikia tarehe 04/07/2017, kulikuwa na jumla ya
maombi 240 ya leseni za utafutaji wa madini (PLs). Kati ya maombi hayo, 86
yalishalipiwa ada ya kuandalia leseni (preparation
fee) na yaliyobaki hayajalipiwa. Kwa taarifa hii, waombaji wote wa leseni za
madini wanatakiwa kukamilisha maombi yao ili yaendane na matakwa ya Sheria ya
Madini ya Mwaka 2010 kama ilivyorekebishwa Mwaka 2017. Hii ni pamoja na:
·
Kulipia ada za
kuandalia leseni za madini (PLs, PMLs, MLs na SMLs) kwa maombi yaliyokidhi
vigezo vya kupewa leseni;
·
Kuwasilisha Local Content Plan kwa mujibu wa
Vifungu vya 102, 103 na 104 vya Sheria ya Madini ya Mwaka 2010
kama ilivyorekebishwa na Sheria ya Marekebisho Anuwai ya Sheria zilizoandikwa,
Sheria Na. 7 ya Mwaka 2017; kwa
waombaji wa leseni za uchimbaji wa kati (MLs) na mkubwa (SMLs) wa madini;
·
Kuwasilisha Corporate Social Responsibility Plan;
na tamko la Integrity Pledge kadri ya
kifungu cha 105 na 106 kwa mtiririko huo wa Sheria ya
Madini ya Mwaka 2010 kama ilivyorekebishwa Mwaka 2017 kwa waombaji wa leseni za
uchimbaji wa kati (MLs) na mkubwa (SMLs) wa madini;
·
Waombaji wote
wa leseni za utafutaji wa madini (PLs) kuwasilisha taarifa za technical resources (Mine equipment, technical personnel,…) na Audited Financial Statements;
·
Waombaji wote
wa leseni za uchimbaji wa kati (MLs) na mkubwa (SMLs) kuwasilisha Cheti cha
Tathmini ya Athari za Mazingira (Environmental
Impact Assessment–EIA Certificate),
taarifa za Feasibility Studies, technical
resources (Mine equipment, technical personnel,…), Audited Financial Statements,
uthibitisho wa tathmini ya fidia na kutokuwepo kwa mgogoro/migogoro katika
eneo linaloombewa leseni ya uchimbaji wa madini; na
·
Waombaji wote
wa leseni za uchimbaji mdogo wa madini (PMLs), baada ya kupata leseni na kabla
ya kuanza shughuli za uchimbaji, wawasilishe Mpango wa Uhifadhi wa Mazingira (Enviromental Protection Plan – EPP );
Nyaraka zote zinazotakiwa, ziidhinishwe na mamlaka
zinazohusika na kuwasilishwa kwa Mtendaji Mkuu wa Tume ya Madini kupitia Sanduku
la Posta 2292, DODOMA.
Imetolewa na:
Prof. Idris Kikula
MWENYEKITI
Mei 11, 2018
0 comments:
Post a Comment