Naibu Waziri Wizara ya Kilimo Dkt. Mary Mwanjelwa akiangalia naomna zoezi la upimaji wa chai ya Wakulima wadogo kama lilivyokuwa likiendeshwa na Wawakilishi wa Kampuni ya NOSC katika mashamba ya Wakulima wadogo wa Kijiji cha Luangu Kata ya Kifanya na Tarafa ya Igominyi katika Wilaya ya Njombe Naibu Waziri Wizara ya Kilimo Dkt. Mary Mwanjelwa akiwa na Mbunge wa Njombe Mwalongo Edward pembeni yao ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Njombe Mji Bwana Edwin Mwenzili na Diwani wa Kata ya Kifanya Nolasco Mtewele
Naibu Waziri Wizara ya Kilimo Dkt. Mary
Mwanjelwa akiwa na Mbunge wa Njombe Mwalongo Edward wakiangalia mche bora wa
parachichi aina ya Hass katika kitalu cha shama la Taasisi ya TAHA katika
Halmashauri ya Mji wa Njombe
Na Mwandishi Maalumu
Naibu Waziri Wizara ya
Kilimo Dkt. Mary Mwanjelwa amewaagiza Kampuni ya NOSC kuendelea kununua kiasi
kikubwa cha Chai ya Wakuliwa wadogo kwanza kabla ya kufikiria kununua kwa
Wakulima wakubwa.
Dkt. Mwanjelwa amesema amefurahishwa
na utendaji wa Kampuni ya NOSC baada ya kujirisha kuwa Kampuni hiyo imekuwa
ikinunua zaidi ya asilimia 80 ya chai ya Wakulima wadogo.
Kampuni ya NOSC ni
Kampuni iliyojikita katika kununua cha ya Wakulima wadogo na wakati huo huo
wanauza chai hiyo kwa Kampuni ya usindikaji wa chai ya Uniliver
Aidha, Dkt Mary
Mwanjelwa amesema Serikali ya Awamu ya Tano kwa nia njema imeamua kuboresha
uzalishaji wa mazao ya kimkakati Chai likiwa zao moja wapo na kwamba maisha ya
Wakulima wanaolima chai yatakuwa bora kama Wakulima hao wataendelea kuwa na
uhakika wa soko na la bei nzuri.
Naibu Waziri aliyasema
hayo wakati wa mkutano wa hadhara mbele ya Wakulima wa chai wa Kijiji cha
Luangu Kata ya Kifanya na Tarafa ya Igominyi katika Wilaya ya Njombe na
kuwahamasisha kuunga mkono juhudi za Serikali kwa kuchangamkia fursa ya kulima
zao la chai ili kuongeza tija na uzalishaji kwa faida yao na Taifa kwa ujumla.
Dkt. Mwanjelwa amesema
kuwa Serikali imeamua kutilia mkazo kwenye kuongeza tija na uzalishaji kwenye
mazao matano ya kimkakati lengo ni kuwasaidia Wakulima kuinua maisha yao na
wakati huohuo kuliongezea taifa akiba ya fedha za kigeni.
Naibu Waziri ameyataja
mazao ya kimkakati kwa ni pamoja na pamba, kahawa, chai, tumbaku na katani.
Katika mkutano huo,
Dkt. Mwanjelwa amewahamasisha Wakulima hao kuongeza eneo la kilimo cha chai kwa
kuwa tayari Serikali imeanza kuboresha miundombinu ya barabara kutoka
mashambani mpaka katika kiwanda cha Uniliver na kuongeza kuwa Taasisi ya
Kizalendo ya NOSC imekuwa mkombozi wa kweli kwa kununua chai yao kwa bei nzuri
ya shilingi 307.11.
Mbali na Taasisi ya
NOSC kununua chai ya Wakulima kwa bei na baadae kuiuza katika Kiwanda cha
Uniliver Taasisi hiyo pia imekuwa ikiwakopesha Wakulima hao pembejeo za kilimo
bila riba kuanzia hatua ya kwanza mpaka ya mwisho na kisha kuwakata baadae
wanapoaza kuvuna chai yao katika kipindi cha miaka mitatu.
Naibu Waziri amewaasa
Wakulima kufuata masharti na elimu ya kilimo cha chai kwa kuwa bila ya kufanya
huvyo wasitarajie matokeo bora.
“Pandeni na mfuate
masharti ya Wataalam ili mpate matokeo bora na kwa kufanya hivyo nasisitiza,
kipaumbele apewe Mkulima mdogo na anayefanya vizuri”. Amekaririwa Dkt
Mwanjelwa.
Naibu Waziri
ameipongeza Kampuni ya NOSC kwa kuwapa kipaumbele Wakulima wazawa ambapo kiasi
cha zaidi ya asilimia 80 ya chai ya Wakulima hao imekuwa ikinunuliwa na kwa bei
ya juu ukilinganisha na maeneo mengine yanayolima chai nchini.
NOSCI ni kifupi cha
maneno Njombe Out – growers Service Company. Ni Kampuni ya Kizalendo ambayo
lengo lake ni kutoa msaada wa kitaalam kwa Wakulima wadogo wa Mkoa wa Njombe
kwa lengo la kuongeza tija na ufanisi kwenye kilimo cha chai na wakati huohuo
kuhakikisha kuwa zao la chai linapandwa na kuendelezwa kwa kufuata utaalam na
kwa kumsaidia Mkulima kupata mazingira wezeshi ya kuendesha kilimo cha chai.
Kampuni ya NOSC
inafanya kazi bega kwa bega na Kampuni ya Uniliver lengo likiwa ni kuhakikisha
walau hekta 3,800 zinapatikana na kuendelezwa na Wakulima wadogo wa chai Mkoani
Njombe.
Dkt. Mwanjelwa amesema
ni vyema Wakulima wa Njombe wakatumia mapato yanayotokana na kilimo cha chai
kuboresha maisha yao.
“Tumieni mapato mnayopata
kwenye chai kuboresha maisha yenu na kwa kufanya hivyo, mtaiweka Njombe kwenye
ramani ya Dunia” Amekaririwa Naibu Waziri.
Wakati huohuo Naibu
Waziri ametumia nafasi hiyo kukitembelea Kituo cha kuhifadhi matunda na
kuyafunga tayari kwa kupeleka nje ya nchi. Kituo kilichojengwa kwa fedha za
Serikali kwa ajili ya kuwasaidia Wakulima wa matunda aina ya parachichi katika
Halmashauri ya Mji wa Njombe.
Dkt. Mwanjelwa amesifu
juhudi zinazofanya na Halmashauri ya Mji wa Njombe kwa kuratibu na kujenga
mazingira mazuri ya kuwaunganisha Wakulima wa matunda hayo na masoko ya
kimataifa yaliyopo Ulaya na Amerika.
Walipokuwa Kituoni hapo
Mbunge wa Jimbo la Njombe Mhe. Edward Mwalongo amewasilisha ombi kwa Naibu
Waziri kuhusu Wakulima wa Jimbo lake kupatiwa miche bora ya zao la parachichi
kama ilivyo kwenye miche ya zao la korosho.
Akijibu ombi hilo Naibu
Waziri amemuagiza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Njombe kutenga fedha za
kutosha kwenye Bajeti yao kwa ajili ya kugharamia shughuli za kilimo na
kusisitiza kuwa Halmashauri zinapaswa kutenga walau asilimia ishirini ya bajeti
zao kwa ajili ya shughuli za kilimo kwa kuwa kilimo kinagusa maisha ya Wananchi
wengi.
MWISHO
0 comments:
Post a Comment