METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, February 25, 2018

BADA YA RUKWA NA KATAVI, NAIBU WAZIRI WA MADINI AWASILI TABORA

Naibu waziri wa wizara ya madini Mhe Doto Mashaka Biteko akisisitiza jambo mara baada ya kutembelea mgodi wa wachimbaji wadogo Kitunda uliopo Wilayani Sikonge, Jana 25 Februari 2018. Picha Zote Na Mathias Canal-Wazo Huru Blog
Naibu waziri wa wizara ya madini Mhe Doto Mashaka Biteko akiwasili katika mgodi wa wachimbaji wadogo Kitunda uliopo Wilayani Sikonge,  Mkoani Tabora, Jana 25 Februari 2018.
Naibu waziri wa wizara ya madini Mhe Doto Mashaka Biteko akizungumza na Sospita Haruna Ibrahimu ambaye anafanya kazi za uchimbaji katika mgodi wa wachimbaji wadogo Kitunda uliopo Wilayani Sikonge, Jana 25 Februari 2018. Mwingine ni Mkuu wa Wilaya ya Sikonge Mhe Peres Boniface Magiri


Na Mathias Canal, Tabora

Baada ya kumaliza ziara ya kikazi katika mikoa ya Rukwa na Katavi Naibu Waziri wa Wizara ya Madini Mhe Doto Mashaka Biteko amewasili Mkoani Tabora ambapo pamoja na mambo mengine atatembelea na kukagua utendaji kazi katika mgodi wa wachimbaji wadogo katika Halmashauri ya Wilaya ya Nzega.

Jana 25 Februari 2018 Mhe Biteko alitembelea mgodi wa wachimbaji wadogo Kitunda uliopo Wilayani Sikonge ambapo alizungumza na wafanyakazi katika mgodi huo ambao una uwezo wa kuajiri wafanyakazi kati ya 5000 mpaka 10,000.

Mhe Biteko aliwaeleza wachimbaji hao kuwa serikali ya awamu ya tano inayoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt. John Pombe Magufuli imekusudia kuondoa manyanyaso kwa wananchi.

Aidha, alielezea mikakati ya serikali katika sekta ya Madini hususani umuhimu wa ulipaji kodi.

MWISHO
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com