METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, February 21, 2018

WAKAZI WA MAGURUWE WAISHUKURU SERIKALI YA AWAMU YA TANO

Wazee wa kimila katika kijiji cha Maguruwe kata ya Bunduki wakimsimika na kumpa heshima maalum Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo.
 Wakazi wa Maguruwe wakimpokea Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo akizungumza na wananchi wa Maguruwe Wilayani Mvomero.
 Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo akilakiwa na wakazi wa Maguruwe wilayani Mvomero.
Wananchi wakicheza ngoma za kiluguru walipompokea Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Selemani Jafo katika kijiji chao.
...........................................................................
Wakazi wa kijiji cha Maguruwe wilayani Mvomero Mkoani Morogoro wameishukuru  serikali ya awamu ya tano kwa kuwathamini na kuweza kufika kwenye kijiji hicho mteule wa Rais ambaye ni Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI Mhe. Selemani Jafo, kwa kuwa hakuna kiongozi wa ngazi ya Uwaziri ambaye amewahi kufika kwenye eneo hilo.

Kutokana na Waziri Jafo kuwa Waziri wa kwanza kufika kwenye kijiji hicho wazee wa kimila wa kijiji hicho walimsimika na kumpa heshima maalum ya waluguru. 

Wakizungumza huku wakiwa wamejawa na furaha, Wananchi hao wamesema kijiji chao ambacho kipo juu kabisa ya safu za milima ya Ulugulu hakuna kiongozi yeyote wa ngazi  ya uwaziri aliyewahi kufika maeneo hayo kwa kuwa barabara zake hazipitiki kirahisi. 

Wamesema wamefurahishwa na kiongozi huyo kwa kuweza kuwafikia walipo hali ambayo imewafanya kujisikia furaha.

Katika ziara hiyo ya kikazi, Waziri Jafo amefanikiwa kuzindua vyumba vitatu vya madarasa vilivyojengwa na Taasisi ya CDTF.

Hata hivyo, kutokana na changamoto kubwa ya barabara katika eneo hilo, Waziri Jafo alimuagiza meneja wa TARURA wilaya ya Mvomero kufanya tathmini ya barabara hiyo ili serikali ione jinsi ya kuifanyia kazi hapo baadae ili wananchi hao waweze kuondokana na adha hiyo.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com