METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, February 22, 2018

WAFUATENI WANANCHI WENYE MIGOGORO YA ARDHI KATIKA MAENEO YAO-MHE MABULA




Na Mwandishi Maalum- Mara

Naibu Waziri wa Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi Angelina Mabula amewaagiza maafisa ardhi na watendaji wa serikali kuhakikisha wanawafuata wananchi wenye matatizo ya ardhi katika maeneo yao ili kutatua migogoro ya ardhi.

Katika kutekeza suala hilo kwa ufanisi, Mabula  amewataka watendaji kutoa matangazo wakati wa kuenda kutatua migogoro ya ardhi kwa kuwaeleza  wanachi ni lini wanaenda katika maeneo yao kuwasikiliza na kwatolea majibu huko waliko.

‘’muende kila kijiji kuwasikiliza wananchi na kutatua kero zao na mnapoenda huko muwatangazie kama siku fulani mtaenda kwa ajili ya kutatua migogoro ya ardhi’’ alisema mabula

Akiwa katika ziara yake katika wilaya ya Butiama mkoani Mara Mabula amewataka watendaji kukaa siku mbili tu ofisini na siku tatu katika wiki wawe maeneo ya tukio kwani serikali inahitaji kumaliza migogoro ya ardhi kwa kuwafuata wananchi huko waliko.

Katika hatua nyingine, naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi Angelina Mabula ameagiza maeneo ya taasisi za serikali kupimwa na kupatiwa hati miliki. Ameshangazwa na baadhi ya halmashauri kushindwa kupima hata taasisi moja ya serikali.

Amesema, katika mazingira kama hayo ya taasisi za serikali kutopimiwa maeneo yao, ni vigumu kabisa kukosekana migogoro na kubainisha kuwa  serikali haitaki kuwabomolea wananchi  kwa kuingia maeneo yasiyo miliki yao na kushauri maeneo ya serikali kuwekewa alama.

‘’kunakuwa na migogoro mingi ya wananchi na umma kwa sababu maeneo mengi hayajapimwa  hivyo nashauri halmashauri zitenge fedha kwa ajili ya kupima maeneo ya umma  na zinaweza  kuanza kupima hata kwa shule na ofiisi za watendaji kadhaa ‘’ alisema Mabula

Pia naibu waziri wa ardhi nyumba na maendeleo ya makazi amesisitiza matumizi ya mfumo mpya wa ulipaji kodi ya ardhi uzingatiwe na kila kitu kifanyike kulingana nilizowekwa.

Aidha,  ameagiza  watendaji kuhakikisha wanasimamia  zoezi zima la utatuaji migogoro ya ardhi  katika maeneo husika kwa kugharamia pesa ya nauli badala ya suala hilo kuachwa kwa walio katika mgogoro kugharamia  kwani linaweza kuwa kichocheo cha rushwa.

Imetolewa na:
Kitengo cha Mawasiliano Serikalini
Wizara ya Ardhi Nyumba na Maendeleo ya Makazi
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com