METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, November 3, 2017

Halmashauri yasimamisha mishahara ya walimu 15

Halmshauri ya wilaya ya Kilosa Morogoro imesimamisha mishahara ya walimu 15 waliohamishwa mwezi Machi bila kulipwa stahiki zao za uhamisho na kupelekea walimu hao kugoma hatua inayodaiwa ni kushindwa kufuata sheria za utumishi wa umma katika kudai.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti walimu wa shule tofauti, Rehema Mkway mwalimu shule ya sekondari Masanze, Isaya Milimi mwalimu shule ya msingi Msimba Kilosa, wamesema walimu wamekuwa wakikabiliwa na changamoto kubwa ya kuhamishwa bila kulipa stahiki zao na kuleta usumbufu na kuvunja morali ya utendaji kazi na kuisababishia serikali madeni yasiyo na msingi.

Akizungumza kwenye mkutano wa Chama cha Walimu Tanzania (CWT) wilaya ya Kilosa  Katibu wa Chama hicho Flora Malomele amesema pamoja na kupatikana mafanikio kadhaa lakini walimu wanakabiliwa na changamoto ikiwemo kutolipwa stahiki zao kwa wakati huku katibu wa tume ya walimu (TSC) Daudi Mchilu akasisitizia watumishi kuzingatia maadili ya utumishi wa umma.

Kwa upande wake Afisa utumishi wa halmashauri ya wilaya ya Kilosa Noel Abeid akijibu madai ya walimu hao  ameahidi kushughulikia suala hilo kwani halmashauri inatafuta fedha na kuwaonya watumishi wa umma kutojichukuliwa sheria mkononi pale wanapoona mwajiri ameenda kinyume cha sheria badala yake wafuate sheria zilizopo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com