METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, November 3, 2017

BARAZA MADIWANI KISHAPU LAPOKEA TAARIFA ZA MIRADI

1
Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu, Stephen Magoiga akizungumza wakati wa kikao cha Baraza la Madiwani kwa ajili ya kupokea taarifa za kata.
2
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Boniphace Butondo akifungua kikao cha Baraza la Madiwani katika ukumbi wa halmashauri.
3
Madiwani wakiimba wimbo wa taifa kabla ya kuanza kwa kikao hicho.
4
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu Boniphace Butondo (kushoto) akiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri, Stephen Magoiga na Makamu Mwenyekiti, Edward Shigela.
…………………………………………………………………………..
Na Robert Hokororo, Kishapu DC

Baraza la Madiwani katika Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga limekutana kwa ajili ya kuwasilisha na kupokea taarifa za miradi ya maendeleo ya kata zake mbalimbali.

Katika kikao hicho cha kujadili taarifa za robo ya kwanza ya Julai hadi Septemba, Mwenyekiti wa halmashauri hiyo, Mhe. Boniphace Butondo aliipongeza Kishapu kwa kupata hati safi kutokana na ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi wa Hesabu (CAG).

Mhe. Butondo ambaye pia ni diwani wa kata ya Lagana aliwataka madiwani waendelee kushikamana na kuwahudumia wananchi katika kata zao ili kueleta maendeleo katika halmashauri ya wilaya hiyo.

Alisema ni wajibu wao kuwahamasisha wananchi kuchangia maendeleo katika kata zao sambamba na kuendelea kuwahamasisha kuhusu kilimo hususan cha mazao yanayostahimili ukame.

“Waheshimiwa tuwahudumie wananchi katika kata zetu na hasa ukizingatia hivi sasa Serikali inapiganaia katika kufufua zao la pamba katika wilaya yetu nasi tuwahamasishe kulima,” alisema.

Aliongeza kuwa katika kikao hicho Baraza linajipima wapi wamefikia katika miradi ya maendeleo na wapi wamekwama hivyo kuweza kutatua changamoto hizo na hatimaye kusonga mbele.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com