METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, November 3, 2017

TRA KWA KUSHIRIKIANA NA MSAMA AUCTION MART WAUWASHA MOTO WA CD FEKI KARIAKOO, MADUKA MENGI YANASWA MTEGONI

01
Bw. Elijah Mwandumbya Kamishna wa Kodi za Ndani Mamlaka ya Mapato Tanzania  (TRA) akizungumza na waandishi wa habari Kariakoo jijini Dar es salaam jana mara  baada ya msako mkali wa wauzaji wa kazi feki za wasanii nchini Tanzania ambapo wamefanikiwa kukamata CD nyingi ambazo hazina stika za TRA na kuonyesha wazi kwamba kazi hizo ni feki,
Kamishna Elijah Mwandumbya amesema wataendelea na kazi hiyo na kuwasaka wote wanaojihusisha na kazi hiyo haramu inayoinyima serikali mapato , lakini pia inayodhulumu jasho la  wasanii nchini Tanzania, Amewashukuru wadau mbalimbali wanaoshirikiana na Mamlaka hiyo katika kufanikisha kazi hiyo na kumpongeza Bw. Alex Msama na kampuni yake ya Msama Auction Mart kwa jinsi ambavyo inajituma na kutetea haki ya wasanii nchini.
1
Bw. Elijah Mwandumbya Kamishna wa Kodi za Ndani Mamlaka ya Mapato Tanzania  (TRA) akizungumza akitoa maelezo kwa mmoja wa vijana walikokamatwa wakiuza kazi feki za wasanii Kariakoo jana.
02
Bw. Alex Msama Mkurugenzi wa  kampuni  ya Msama Auction Mart akikamata moja ya kompyuta ambazo zinatumika kutoa kopi feki za nyimbo na filamu za wasanii huku mmoja wa vijana wanaojihusisha na kazi hiyo akiwa chini ya ulinzi.
3
Bw. Elijah Mwandumbya Kamishna wa Kodi za Ndani Mamlaka ya Mapato Tanzania  (TRA)  akitoa maagizo  kwa mmoja wa vijana walikokamatwa wakiuza kazi feki za wasanii Kariakoo jana.
6
Bw. Alex Msama Mkurugenzi wa  kampuni  ya Msama Auction Mart akiongozana na Bw. Elijah Mwandumbya Kamishna wa Kodi za Ndani Mamlaka ya Mapato Tanzania  (TRA) wakati walipofanya msako huo Kariakoo jijini Dar es salaam jana.
7
Mmoja wa watuhumiwa wanaojihusisha na kazi hiyo akijijitetea mbele ya askari wakati alipkamatwa katika duka lake akiuza CD feki za nyimbo na filamu.
8
Bw. Alex Msama Mkurugenzi wa  kampuni  ya Msama Auction Mart akionyesha moja ya CD feki zilizokamatwa katika moja ya duka kwa maofisa wa TRA.
9
Watuhumiwa wa uuzaji wa CD feki za Muziki na Filamu wakiwa chini ya Ulinzi na maboksi ya CD zao mara baada ya kufikishwa kwenye kituo Kikuu cha cha polisi kanda maalum ya Dar es salaam.
10
Mmoja wa maaskari akiimarisha ulinzi kwa watuhumiwa hao katika kituo kikuu cha Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com