Raila Odinga akizungumza hivi karibuni katika jumba la siasa la Chatham jijini London nchini Uingereza Oktoba 13 2017
Kiongozi wa muungano wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga amesema
yuko tayari kufanya mazungumzo na rais Uhuru Kenyatta kuhusu kufanyika
kwa Uchaguzi utakaokuwa huru na haki wala sio namna ya kuunda serikali
ya muungano kama inavyodaiwa na rais Uhuru Kenyatta na Naibu wake
William Ruto.
Chanzo:RFI
“Niko tayari kuzungumza na rais Kenyatta
kuhusu namna ya kuwa na Uchaguzi utakaokuwa huru na haki sio kuunda
serikali ya muungano,” alisema Odinga.
Aidha, amesisitiza kuwa hatawania
wadhifa wa urais katika Uchaguzi uliopangwa kufanyika tarehe 26 mwezi
huu bila ya mabadiliko ndani ya Tume ya Uchaguzi.
Rais Kenya na Naibu wake, wamekuwa
wakimshutumu Odinga kwa kujiondoa kwenye Uchaguzi huo kwa sababu anataka
kuundwa kwa serikali ya muungano.
Mbali na hilo, Mahakama ya Juu nchini
Kenya imeamua kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Wafula Chebukati, hana
mamlaka ya kubadilisha matokeo ya Uchaguzi wa urais.
Tume ya Uchaguzi ilikwenda katika
Mahakama hiyo kutaka kufahamu jukumu la Mwenyekiti wa Tume hiyo, baada
ya matokeo ya urais ya mwezi Agosti kufutwa.
Nayo Mahakama Kuu imeondoa kwa muda
marufuku iliyokuwa na serikali kuzuia maandamano ya wafuasi wa upinzani
katikati ya miji ya Nairobi, Mombasa na Kisumu.
Upinzani ulienda Mahakamani kutaka
kuondolewa kwa marufuku hayo, kwa kile walichosema kuwa ni kinyume na
haki za waandamanaji na Katiba ya Kenya.
0 comments:
Post a Comment