Habari ndugu msomaji wa makala haya na msaka mafanikio? Ni matumaini
yangu makubwa u mzima wa afya tele na unaendelea na michakato yako ya
kila siku. Kwa upande wangu mimi ni mzima wa afya tele, naendelea vyema
na pilikapilika za kila siku ili kuhakikisha mafanikio makubwa yanakuwa
upande wangu.
Nichukue fursa hii adhimu na kwa moyo mkunjufu kuweza kukukaribisha
tuweze kujifunza kwa pamoja kuhusu ukuaji wa kibiashara hususani katika
suala zima la mahusiano bora kati yako na mteja wako.
Kimsingi ni kwamba biashara yeyote ile ni mjumuisho kati ya
mfanyabiashara na mteja. Pindi inapotokea mtafaruku kati yao,
mfanyabiashara hali yake huwa ni ngumu kibiashara. Lakini kinyume chake
ni kwamba pindi pawapo na mahusiano mazuri kati ya mfanyabiashara na
mteja, mfanyabiashara huneemeka kutoka kwa mteja huyo.
Lakini Ukichunguza kwa umakini kati ya mfanyabiashara na mteja utagundua
ya kwamba mteja huwa ni mtu wa kujishusha sana pindi akutanapo na
mfanyabiashara katika suala zima la kubadilishana huduma. Hata ule usemi
usemao mteja ni mfalme hukaa kushoto kwa wakati huo.
Ndio maana mteja akienda kununua kitu fulani atasema naomba kitu fulani
na mwisho siku mteja huyo atatoa na hela licha ya kutanguliza neno.
Lakini pamoja hayo wapo wafanyabiashara ambao wamekuwa wakiwafukuza
wateja wao bila wao wenyewe kujua.
Na kutatokea kwa hali kumesababishwa biashara nyingi kudolola huku
chanzo ikiwa mfanyabiashara mwenyewe. Unakuta mfanyabiashara hata
"biashara kauli" hata siku moja, Ukichunguza kwa umakini itaniunga
mkono kwa hiki ninachosema.
Hivi hujawahi kwenda dukani ukakuta mhudumu hana muda na wewe? Achilia
mbali hilo hivi hujawahi kwenda dukani kwa ajili ya kupata huduma fulani
ukajibiwa vibaya? Bila shaka hilo litakuwa si geni Kwako. Sasa
tujiulize huo usemi usemao mteja ni mfalme upo wapi sasa? Bila shaka
haupo.
Hivyo kwa kuwa unataka kukua kibiashara huna budi kujenga utamaduni bora
na mahusiano mazuri kati yako na mteja wako. Kwani kutokuwepo kwa
mahusiano mazuri ya mteja na mfanyabiashara na chanzo kikubwa cha kufa
kibiashara.
Hapa ndipo ambao huwa nakumbuka mwalimu wangu wa ‘personal brand’
Charles Nduku siku moja aliwahi kuniambia ya kwamba "ukimuhudumia mteja
mmoja vizuri mteja huyo anauwezo wa kukuletea wateja wapya kumi, lakini
ukimuhudumia vibaya mteja mmoja anauwezo kuwapoteza wateja wapya kumi na
kuwazuia wateja wengine watano uliowazoea. Hapo sasa inakubidi uchague
mwenyewe".
Hapo ndipo nikagundua ya kwamba mteja mmoja ana thamani kubwa sana
katika biashara yako. Hivyo mteja mpya ambaye atakuja kwako leo kwa
ajili ya kupata huduma yeyote ile, hakikisha ya kwamba humpotezi, kwani
mteja huyo ana uwezo wa kuja na wateja wapya wengi endapo utamhudumia
vizuri.
Haya ni baadhi ya maneno ambayo yatamfanya mteja wako ajisikie vizuri zaidi:
# Karibu sana jisikie upo nyumbani.
# Samahani sijui unahitaji/ tukuhudumie nini.
# Karibu tena kwetu mteja ni mfalme.
# Asante sana na karibu tena.
# Kwa chochote usisite kuwasiliana nasi kupitia mawasiliano yetu.
Pia kama una uwezo wa kumpa mteja wako zawadi pindi anunuapo bidhaa au
huduma jaribu kufanya hivyo kwani kitendo hicho humfanya mteja asihame
kwenda kupata huduma sehemu nyingine. Pia kufanya hivyo humfanya mteja
ajione yeye ni wa thamani sana mbele yako.
Saturday, October 28, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi. ...
-
📌 Asema Rais, Dkt. Samia anafanya kazi kubwa ya kuwaunganisha Watanzaia 📌 Atak...
-
Mvua kubwa za El-Nino zilizonyesha zimeleta athari maeneo mbalimbali...
-
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipokea hundi ya sh. 4, 000,000,000/= kutoka kwa Meneja Mkazi (Country Manager) wa Kampuni ya Madini ya...
-
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akisisitiza jambo wakati akifungua kikao kazi cha vyama vya ushirika kuhusu ununuzi wa mbolea k...
Powered by Blogger.
0 comments:
Post a Comment