METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, September 25, 2017

RC NDIKILO- UPATIKANAJI WA TAKWIMU SAHIHI KATIKA SEKTA YA KILIMO UTALETA MAPINDUZI YA KIMAENDELEO

SAM_5685
Mkuu wa mkoa wa Pwani ,mhandisi Evarist Ndikilo ,akifungua mafunzo ya siku tano ya wadadisi wa utafiti wa kilimo mwaka 2016/2017 ,yaliyoandaliwa na ofisi ya takwimu taifa (NBS). Picha na Mwamvua Mwinyi
………………
Na Mwamvua Mwinyi, Pwani

SERIKALI mkoani Pwani,imetoa rai kwa watendaji ,wenyeviti wa mitaa/vijiji na wataalamu kuhakikisha wanashirikiana na wadadisi na wasimamizi watakaofanya kazi ya utafiti wa kilimo mwaka 2016/2017,ili kupata takwimu halisi .

Hatua hiyo itasaidia ,kupanga mipango ya maendeleo katika sekta ya kilimo ambayo inaajiri zaidi ya asilimia 75 ya watanzania hasa katika maeneo ya vijijini.

Akifungua mafunzo ya siku tano ya wadadisi wa utafiti wa kilimo mwaka huu wa fedha,mkuu wa mkoa wa Pwani mhandisi Evarist Ndikilo,alisisitiza endapo utakuwepo ushirikiano mzuri utawezesha kuweka mikakati ya baadae ya kimkoa na taifa.

Aidha aliwaomba wananchi kutoa ushirikiano wa kutosha  kwa wadadisi na wasimamizi hao ili kutoa taarifa sahihi kuhusiana na utafiti.

Mhandisi Ndikilo,alieleza kwa mujibu wa sheria ya takwimu namba 9 ya mwaka 2015 taarifa zitakazokusanywa zitatunzwa kwa usiri na zitatumika kusimamia kupatikana takwimu halisi za kilimo.
Alisema,sekta ya kilimo ina mchango mkubwa kwenye uchumi wa nchi ambapo mwaka 2016 mchango wa sekta hiyo pato la taifa ulikuwa asimilia 29.1 

”kati ya asilimia hiyo kilimo cha mazao kilichangia asilimia 15.5,“Mifugo asilimia 7.7 ,misitu asilimia 3.9 na sekta ya uvuvi ilichangia asilimia 2.0 “alisema mhandisi Ndikilo.

Mkuu huyo wa mkoa alisema,mafunzo hayo ni hatua muhimu katika,utekelezaji wa mipango ya kuboresha maisha ya watanzania.
Mhandisi Ndikilo,alifafanua serikali imeandaa mipango madhubuti ya muda mfupi na mrefu inayolenga katika kuimarisha uchumi na kuondoa umaskini ikiwa ni pamoja na dira ya taifa ya maendel;eo ya mwaka 2025 .

Alisema ,hivyo serikali na wadau bado inaendelea kuhitaji takwimu rasmi kwa ajili ya kupanga utekelezaji na kutathmini program mbalimbali za maendeleo ya kitaifa ,kikanda na kimataifa .

Dira ya taifa ya  maendeleo ya mwaka 2025 na mpango wa pili wa taifa wa maendeleo wa miaka mitano unaoanza kutekelezwa mwaka huu wa fedha.

Mhandisi Ndikilo,alibainisha kuwa,baada ya kukamilika kwa utekelezaji wa malengo ya millennia ya mwaka 2015 Tanzania na dunia kwa ujumla.

Aliishukuru serikali ya Marekani kupitia shiriki lake la mendeleo ya kitaifa USAID kwa msaada wa kiufundi na fedha uliowezesha kufanikisha utafiti .

Mtakwimu kutoka ofisi ya takwimu taifa (NBS),ambae pia ni mratibu wa mafunzo hayo kanda ya Mashariki, Theresia Sagamilwa,alisema mafunzo yanafanyika kikanda ,ambapo kanda hiyo inahusisha mkoa wa Pwani,Lindi,Mtwara na Dar es salaam.

Alisema lengo kuu la mafunzo hayo ,ni kukusanya taarifa za uzalishaji kwa kilimo na ufugaji kwa mwaka wa kilimo uliopita.

Theresia alieleza,utafiti unafanyika nchi nzima ,”na wanaomaliza mafunzo ya udadisi wataenda kwenye mikoa yao uhusika kuendelea na zoezi la utafiti.

Mdadisi kutoka Lindi,Makenza Matola alishukuru kupatiwa mafunzo ambayo yatawasaidia kufanya zoezi la udadisi kwa kina na kujua uzalisha wa kilimo kwa kipindi kilichopita.

Sensa ya kilimo huwa ikifanyika baada ya miaka kumi lakini kwa sasa imerahisishwa ambapo kunafanyika utafiti wa kilimo na mifugo kila mwaka.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com