METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, December 23, 2021

RAIS MHE. SAMIA SULUHU HASSAN AKABIDHI ZAWADI MBALIMBALI ZA SIKUKUU YA KRISMASI NA MWAKA MPYA KWA MAKUNDI MAALUMU DAR ES SALAAM

 

Msaidizi wa Rais (Mnikulu) Bw. Said Ali Juma akikabidhi Mbuzi, Mafuta ya kupikia pamoja na Mchele kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwenye Kituo cha Nyumba ya Amani na Furaha (Missionaries of Charity Mother Teresa Children’s Home) kilichopo Mburahati Jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kusherehekea Sikukuu ya Krismasi na Mwaka Mpya leo tarehe 23 Desemba, 2021.

 

Msaidizi wa Rais (Mnikulu) Bw. Said Ali Juma akikabidhi Maziwa, sabuni pamoja na pampers za watoto kwa niaba ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, kwa Mlezi wa Kituo cha Kulea Watoto wanaoishi katika Mazingira Hatarishi cha Msimbazi Centre Jijini Dar es Salaam Sister Stella Selugenge leo tarehe 23 Desemba, 2021. PICHA NA IKULU

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com