METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, September 12, 2017

MPANGO WA TAIFA WA USIMAMIZI WA TAKWIMU ZA AFYA WAZINDULIWA RASMI

pix 1
Katibu Mkuu Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto (Wizara ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya akiongea na wadau mbalimbali wa sekta ya Afya hawapo pichani wakati wa uzinduzi wa mpango wa Taifa wa usimamizi wa Takwimu za Afya uliofanyika jijini Dar es salaam.
pix 2
Katibu Mkuu Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto (Wizara ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya katikati akiongoza wadau mbalimbali wa sekta ya ya afya  wakishikana  mikono na kunyosha juu kuashiria kuzindua rasmi wa mpango wa Taifa wa usimamizi wa Takwimu za Afya uliofanyika jijini Dar es salaam.
pix 3
Wadau mbalimbali wa sekta ya afya wakishikina mikono kwa pamoja wakiongozwa na Katibu Mkuu Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto (Wizara ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya hayupo pichani kuashiria na   kuzindua rasmi wa mpango wa Taifa wa usimamizi wa Takwimu za Afya uliofanyika jijini Dar es salaam.
pix 4
Katibu Mkuu Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto (Wizara ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya katikati waliokaa akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya  Wadau mbalimbali wa sekta ya afya wakati wa uzinduzi wa mpango wa Taifa wa usimamizi wa Takwimu za Afya uliofanyika jijini Dar es salaam.
pix 5
Wadau mbalimbali wa sekta ya afya wakifuatilia kwa makini hotuba ya  Katibu Mkuu Wizara ya Afya ,Maendeleo ya Jamii,Jinsia Wazee na Watoto (Wizara ya Afya) Dkt. Mpoki Ulisubisya hayupo pichani wakati wa uzinduzi wa mpango wa Taifa wa usimamizi wa Takwimu za Afya uliofanyika jijini Dar es salaam. Picha Na WAMJW.
…………………………
NA WAMJW-DAR ES SALAAM

MPANGO wa Taifa wa usimamizi wa Takwimu za Afya umezinduliwa rasmi ili kuweka kumbukumbu  sahihi za taarifa za afya zinazosaidia katika kufanya tathimini, kupanga, na kufanya maamuzi juu ya uboreshaji wa huduma za afya nchini.

Akiongea na wadau mbalimbali wa afya jijini Dar es salaam wakati wa uzinduzi huo Katibu Mkuu Wizara ya Afya Dkt. Mpoki Ulisubisya amesema kuwa Mpango huo utasaidia Serikali na wadau mbalimbali wa sekta ya afya kufanya utekelezaji bora  kutokana na vipaumbele vilivyowekwa kupitia takwimu za nchi.

“Mpango huu utaiwezesha nchi kulingana na mpango wa pamoja kwa kuweka vipaumbele ili kuwaleta pamoja wadau wote wa maendeleo katika sekta ya afya nchini “ alisema Dkt. Ulisubisya.

Aidha Dkt. Ulisubisya amesema kuwa Tanzania imekuwa nchi ya tatu kusini mwa jangwa la sahara barani Afrika kuzindua mpango huo ikitanguliwa na nchi jirani za Kenya na Malawi.

Mbali na hayo Dkt. Ulisubisya amesema kuwa wanategemea pia nchi zilizoendelea, taasisi na Mashirika ya kimataifa  watakuwa tayari kuchangia mpango huo ili kuweza kufikia malengo ya nchi waliyoweka.
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com