Rais
wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania, Wallace Karia amewateua
Makamu wa Rais wa zamani wa TFF, Athuman Nyamlani na Ahmed Mgoyi kuwa
Wajumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF. Rais Karia ameteua kwa kwa mujibu
wa mamlaka aliyonayo katika Katiba ya TFF ikiwa ni wiki moja baada ya
kupatikana kwa viongozi wa shirikisho katika uchaguzi mkuu uliofanyika
Agosti 12, mwaka huu.
Rais
Karia aliwatambulisha viongozi hao kwenye Kikao cha Kamati ya Utendaji
iliyofanyika Jumanne Agosti 22, mwaka huu jijini Dar es Salaam. Katika
kikao hicho pia Rais Karia alitumia fursa hiyo kutangaza viongozi wa
kamati mbalimbali za TFF zikiwamo za kinidhamu na kisheria.
Kamati ya Nidhamu: Mwenyekiti Tarimba Abbas, Makamu Mwenyekiti, Peter Hella wakati wajumbe ni Boniface Lyamwike, Dk. Bill Haonga na Kassim Dau.
Kamati ya Rufani za Nidhamu:
Mwenyekiti ni Wakili Rahim Zuber Shaban; Makamu Mwenyekiti, Stella
Mwakingwe wakati Wajumbe ni Abbas Mtemvu, Amani Mulika na Siza Chenja.
Kamati ya Maadili:
Mwenyekiti ni Wakili Hamidu Mbwezeleni, Makamu Mwenyekiti ni Wakili
Steven Zangira wakati Wajumbe ni Glorious Luoga, Walter Lungu na Amin
Bakhressa.
Kamati ya Rufaa ya Maadili:
Mwenyekiti ni Wakili Ebenezer Mshana; Makamu Mwenyekiti ni DCP.
Mohammed Mpinga na wajumbe ni Wakili Benjamin Karume, George Mayawa na
ASP. Benedict Nyagabona.
Kamati ya Uchaguzi:
Mwenyekiti ni Revocatus Kuuli; Makamu Mwenyekiti ni Wakili Mohammed
Mchengerwa; Wakili Edwin Mgendera; Wakili Kiomoni Kibamba na Wakili
Thadeus Karua.
Kamati ya Rufani ya Uchaguzi: Mwenyekiti
ni Kenneth Mwenda; Makamu Mwenyekiti ni Jabir Shekimweri na Wajumbe ni
Wakili Rashid Sadalla, Irene Kadushi na Mohammed Gombati.
Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji: Mwenyekiti
ni Elias Mwanjala; Makamu Mwenyekiti ni Wakili Malangwe Mchungahela
wakati Wajumbe ni Zakaria Hanspope, Robert Selasela, Goodluck Moshi,
Mhandisi Issa Batenga na Hamis Semka.
Kamati ya Fedha na Mipango:
Mwenyekiti ni Michael Wambura; Makamu Mwenyekiti ni Francis Ndulane na
Wajumbe ni Almas Kasongo, Pascal Kihanga, Maximillian Tabonwa, Paul
Bilabaye na Farid Abeid.
Kamati ya Mashindano:
Mwenyekiti ni Ahmed Mgoyi; Makamu Mwenyekiti ni James Mhagama wakati
Wajumbe ni Kenneth Pesambili, Shafii Dauda, Fortunatus Kalewa na
Mhandisi Andrew Makota.
Kamati ya Ufundi: Mwenyekiti
ni Vedastus Lufano; Makamu Mwenyekiti ni Issa Bukuku na wajumbe ni
Sarah Chao, Ally Mayay, Michael Bundala, Omar Abdulkadir na Israel
Mujuni.
Kamati ya Soka la Vijana:
Mwenyekiti ni Khalid Abdallah; Makamu Mwenyekiti ni Lameck Nyambaya na
Wajumbe ni Mohammed Aden, Ramadhani Nassib, Salim Kibwana na Vicent
Majili.
Kamati ya Mpira wa Wanawake:
Mwenyekiti ni Amina Karuma; Makamu Mwenyekiti ni Rose Kissiwa na Katibu
wa Kamati hiyo ni Somoe Ng’itu wakati Wajumbe ni Zena Chande, Beatrice
Mgaya, Sofia Tigalyoma, Zuhura Kapama na Nia Mjengwa.
Kamati ya Waamuzi: Mwenyekiti ni Saloum Chama; Makamu Mwenyekiti Joseph Mapunda wakati Wajumbe ni Nassib Mabrouk, Leslie Liunda na Soud Abdi.
Kamati ya Habari na Masoko:
Mwenyekiti ni Dunstan Mkundi; Makamu Mwenyekiti ni Mbasha Matutu wakati
Wajumbe ni Imani Kajura, Mgaya Kingoba, Godfrey Dilunga na Samson
Mbamba.
Kamati ya Ukaguzi wa Fedha:
Mwenyekiti ni Yahya Hamad; Makamu Mwenyekiti ni Athuman Nyamlani na
Wajumbe ni Khalifa Mgonja, Japhary Kachenje, Jackson Songoro na Benesta
Rugora.
Kamati ya Tiba: Mwenyekiti
ni Dkt. Paulo Marealle; Makamu Mwenyekiti ni Dkt. Fred Limbanga Wakati
wajumbe ni Dkt. Norman Sabun, Dkt. Lisobina Kisongo, Dkt. Eliezer
Ndalama, Dkt. Elson Maeja na Violet Lupondo.
Kamati ya Futsal na Beach Soccer:
Mwenyekiti ni Ahmed Mgoyi; Makamu Mwenyekiti ni Hussein Mwamba na
Wajumbe ni Blassy Kiondo, Isaac Munisi, Didas Zimbihile na Aaron Nyanda.
Kamati ya Ajira: Mwenyekiti
ni Issa Bukuku; Makamu Mwenyekiti ni Saloum Chama wakati Wajumbe ni
Athuman Kihamia, Mtemi Ramadhani, Noel Kazimoto na Hawa Mniga.
Kamati ya Leseni za Klabu:
Mwenyekiti ni Wakili Lloyd Nchunga; Makamu Mwenyekiti Wakili Emmanuel
Matondo wakati Wajumbe ni Profesa Mshindo Msolla, Hamisi Kissiwa na
David Kivembele.
Kamati ya Rufaa za Leseni:
Mwenyekiti Wakili Dk. Damas Ndumbaro; Makamu Mwenyekiti ni Wakili Alex
Mngongolwa Wajumbe ni Meneja wa zamani wa Uwanja wa Taifa, Charles
Matoke, Tumainiel Mlango na Ahmed Menye.
0 comments:
Post a Comment