METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, August 26, 2017

UVCCM WAFANYA USAFI OFISI YA DC CHAMWINO

Kwa Heshima Kubwa Vijana wa UVCCM leo wameshiriki Kufanya Usafi Pamoja na DC Mama Vumilia Nyamoga wa Chamwino akiwa na Wasaidizi wake DAS na Afisa Tarafa wa Chilonwa Ndg Mfaki na Maafisa Wengine.

Akizungumza na Vijana DC amewasisitizia Vijana Kuhakikisha Wanajitolea zaidi ktk Shughuli zakijamii ili Kujifunza na Kujenga Network yao kwani Ndio Mirango ya Fulsa kwao.

Nao Vijana wameahidi Ushirikiano kwa Chama na Serikali hii ya Awamu ya Tano, kwani wanayo imani Kubwa na Utendaji Kazi Wa Awamu Hii Kuanzia kwa Rais mpaka Kwa Watendaji wa Ngazi ya Chini Kabisa.

Nae Katibu wa Vijana Wilaya ya Chamwino Ndg Peter Dafi Akishukuru kwa Niaba ya Vijana UVCCM Chamwino, Amesema Kazi Kubwa ya Vijana Nikuhakikisha Wanayafanya yale Yote ambayo Vijana wanapaswa Kuyafanya kwa Umri wao wa Ujana kwani Vijana ni Taifa La Leo na Vijana Ni Jeuri ya Chama.
Ivo kwa hali na Mali, Kwa Shida na Raha Tutakitumikia Chama Cha Mapinduzi na Serikali yake.
Dafi amemuahidi DC kumpatia Ushirikiano wa Kila Namna ili Kujenga Chamwino Bora na Taifa Moja lenye Amani na Upendo Ili Kuishi kwa amani na Furaha tele.

#ChamwinoYetu
#TanzaniaYetu
#UzalendoKwanza
#HapaKaziTu

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com