METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, August 28, 2017

CCM YAFUTA UCHAGUZI WA KATA 44

 Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Ndg Humphrey Polepole

Na Mathias Canal, Dar es salaam

Chama Cha Mapinduzi Kimefuta Uchaguzi katika Kata 44 kati ya kata 3727 zilizofanya Uchaguzi katika ngazi Mbalimbali kutokana na kukiuka taratibu za Uchaguzi ikiwa Ni ishara ya Kuelekea kuwa na CCM mpya na Tanzania Mpya.

Kufutwa kwa uchaguzi katika Kata hizo Ni matokeo ya ukiukwaji wa Kanuni za Uchaguzi na katiba ya CCM, kuendeleza makundi baada ya Uchaguzi, Kupanga safu za Uongozi kwa maamuzi ya Nani awe kiongozi Jambo ambalo Ni kinyume na utaratibu wa Uchaguzi.

Akitangaza Kufutwa kwa uchaguzi katika Kata hizo mbele ya waandishi wa habari katika mkutano uliofanyika katika Ukumbi mdogo wa CCM wa (OND)-Lumumba Katibu wa NEC, Itikadi na Uenezi Ndg Humphrey Polepole alisema kuwa hiyo Ni Awamu ya kwanza ya kufanya maamuzi lakini wale wote waliosababisha kadhia hiyo watachukuliwa Hatua kwa mujibu wa taratibu za Chama.

Alisema kuwa wapo wagombea wengine walipokuwa Viongozi katika Awamu zilizopita walishindwa kutoa usimamizi wa Mali za Chama lakini bado wamerejeshwa katika uongozi huku wengine wakiwa si wakazi wa maeneo husika walipoomba nafasi za Uongozi.

Sababu nyingine Ni pamoja na baadhi ya maeneo wajumbe wa vikao kutopewa taarifa sahihi za wagombea Jambo ambalo lilipelekea kuchagua viongozi wasiokuwa na sifa.

Polepole alisema kuwa Kwa mujibu wa Katiba ya Chama Cha Mapinduzi imetoa mamlaka kwa Katibu Mkuu kutoa Maelekezo ya kufuta Uchaguzi kwa mashauriano na Mwenyekiti wa CCM hivyo kupitia mashauriano Kati ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli na Katibu ya Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Ndg Abdulrahiman Kinana kufuta Uchaguzi na kuagiza kurejea upya Uchaguzi huo baada ya kusikiliza malalamiko na kero za kiuchaguzi.

Polepole alizitaja kata hizo kuwa ni Buguruni, Liwiti, Kariakoo, Manzese, Makuburi, Mabibo, Kigamboni, Kiburugwa, Mchafukoge, Gerezani, Segerea, Pugu, Pugu Stesheni, Ilala, Kijitonyama (Tawi la Mwenge), Mbagala kuu,  Mianzini, Ndugumbi, Kilungule, Makumbusho, Kitunda, Ukonga, na Msasani katika Mkoa wa Dar es salaam.

Nyingine Ni Kata ya Mapinga iliyopo Mkoa wa Pwani, Kata ya Lumemo Mkoani Morogoro, Kata zote 18 za Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara sambamba na Kata ya Seria kwa vijana iliyopo Kondoa Vijijini Mkoani Dodoma.

Polepole alitoa Rai kwa Viongozi wote wa Chama Cha Mapinduzi na Jumuiya zake kuendelea kusimamia katiba, Kanuni na maadili katika kipindi chote Cha Uchaguzi wa ndani wa Chama kwa kupiga Vita rushwa kadhalika na ubadhilifu wa Mali za umma.

Alisema kuwa CCM inaongozwa kwa mujibu wa Katiba na kanuni hivyo kama kuna kiongozi atabainika kukiuka taratibu na maadili ya Chama atachukuliwa Hatua ya kuhojiwa na kamati ya maadili na kupitia vikao Hatua stahiki zitachukuliwa dhidi yake.

Aliongeza kuwa Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli anawakumbusha watendaji wa chama katika ngazi zote kuzingatia, katiba, kanuni na kutenda haki kwa kila kutakopokuwepo na malalamiko, yasikilizwe na kutatuliwa kwa wakati kwani kwa mujibu wa katiba na kanuni viongozi na watendaji watakaoshindwa kushughulikia kero ya malalamiko kwa wakati watalazimika kuwajibika kama viongozi na watendaji

MWISHO

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com