Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. George B.
Simbachawene (Mb) akitoa maelekezo kwa Mhandisi Geophrey Mwamkinga na Wataalam
wengine juu ya marekebisho ya barabara ya Lumuma hadi Mbuga yenye urefu wa
kilomita 21 ambapo alimtaka kuchukua hatua kwa mkandarasi kampuni ya M/S Besta
Holding Co Ltd ya Jijini Dar es Salaam kufanya marekebisho ya upanuzi wa
barabara, kumwaga kifusi kisicho tereza, kujenga kingo imara za barabara na
marekebisho maalum sehemu korofi kabla ya msimu wa mvua.
Waziri
wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. George B.
Simbachawene (Mb) akitoa maelekezo kwa Mhandisi Geophrey Mwamkinga na Wataalam
wengine juu ya marekebisho ya barabara ya Lumuma hadi Mbuga yenye urefu wa
kilomita 21 ambapo alimtaka kuchukua hatua kwa mkandarasi kampuni ya M/S Besta
Holding Co Ltd ya Jijini Dar es Salaam kufanya marekebisho ya upanuzi wa
barabara, kumwaga kifusi kisicho tereza, kujenga kingo imara za barabara na
marekebisho maalum sehemu korofi kabla ya msimu wa mvua.
Na Fred Kibano, Mpwapwa
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Tawala
za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. George B. Simbachawene (Mb) amemwagiza
Msimamizi wa Wakala wa barabara za Vijijini (TARURA) Mhandisi Geophrey
Mwamkinga kuhakikisha barabara ya Lumuma hadi Mbuga wilayani Mpwapwa
inatengenezwa kwa kiwango kinachotakiwa na kwa thamani halisi ya fedha za
Serikali.
Mheshimiwa Simbachawene ameyasema
hayo akiwa katika ziara ya kutembelea Mamlaka za Serikali za Mitaa ngazi ya
vijiji kujionea maendeleo ya vijiji katika sekta za Afya, Elimu, Maji, Ardhi na
eneo la Utawala bora ngazi ya vijiji.
Amesema Mkandarasi anayejenga
barabara hiyo kampuni ya M/S Besta Holding Co Ltd ya Jijini Dar es Salaam bado
haijafanya kazi nzuri ijapokuwa ujenzi wake umefikia asilimia 70 kwani wembamba
wa barabara hiyo ambao hauruhusu magari kupishana, kuwa na mitaro midogo ya
kutupa maji, uvunjaji wa miamba kwa mita chache pembeni mwa barabara hiyo ya
milima ya Kizi haujafanyika ipasavyo, ikiwa ni pamoja na mitaro ya kinga mita
kwa pembeni na kujaza kifusi ambacho hakitelezi.
“Kwa hiyo, barabara lazima
itanuliwe, mlima huu hapa hakati, huyu jamaa (Mkandarasi), anagusagusa tu
lakini hakati, Yule mwenzake wa kule Wotta (kata nyingine wilayani Mpwapwa)
anakata, tena ni jiwe tu kutoka chini, yeye huyu ni udongo anafanya hivi,
lakini hakati (mlima kwa upande wa pembeni), hivi vifereji ni utapeli mtupu,
hivi vifereji wakati wa mvua vitaondoka vyote kwa sababu hujaandaa vizuri njia
yenyewe, ukijenga mfereji unacheza (ni kama utani)”
Barabara ya kata za Lumuma na Mbuga
yenye urefu wa kilomita 21 inahusisha matengenenezo makubwa, ni barabara ya
siku nyingi ambayo haikuwahi kuwa chini ya Halmashauri ambapo ni wananchi
pekee na Wamisionari wa Kanisa katoliki ndio walioianzisha na kuikarabati
kuweza kupita kwa shughuli zao.
Mradi huo mkubwa wa ukarabati wa
barabara ulianza mapema mwezi Februari, 2017 na kutarajiwa kwisha katikati ya
mwezi Agosti, 2017 na jumla ya gharama zitakazotumika ni shilingi 641,912,684
na mpaka sasa amekwishalipwa asilimia 33 ya fedha zote.
Kwa mujibu wa Bw. Mwamkinga mpaka
sasa mkandarasi huyo amekwishalipwa kiasi cha shilingi 209,175,882 na bado
shilingi 432,736,802. Pia mkandarasi ameongezewa muda wa siku 60 kutokana
na changamoto za kijiografia zinazosababisha vifaa kutofika kwa wakati na
kufanya ufuatiliaji kwa kuweka vikao kazi kwa kila wiki kuona maendeleo na
ubora wa kazi na kutoruhusu ucheleweshaji mwingine wa kazi kabla ya msimu ujao
wa mvua.
Mheshimiwa Simbachawene anafanya
ziara katika Mamlaka za Serikali za Mitaa hasa maeneo ya vijijini ili kujionea
hali halisi ya utendaji, migogoro ya ardhi, utunzaji wa mazingira, huduma kwa
wananchi na ukamilishaji wa miradi ya maendeleo ambapo mwishoni mwa wiki
ametembelea kata za Mbuga, Kibakwe na Ipera zenye vijiji kadhaa wilayani
Mpwapwa kama sehemu ya kazi zake za kujionea maendeleo ya wananchi na kero zao.
0 comments:
Post a Comment