METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, November 4, 2019

DKT TULIA AENDELEA KUIIMARISHA CCM MKOANI MBEYA






November 2, 2019 Naibu Spika Dkt. Tulia Ackson alikuwa Mgeni rasmi katika Tamasha la kuimarisha Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM mkoa wa Mbeya lililofanyika katika viwanja vya Sokoine ambapo kupitia taasisi yake ya Tulia Trust ametoa michango mbalimbali kwa makundi tofauti yalishoshiriki katika tamasha hilo.

Miongoni mwa michango hiyo ni pamoja na kituo cha Afya cha Makongolosi Chunya ambacho kimepata Shilingi Milion tano (Tsh 5,000,000/-), Umoja wa Wanawake Tanzania mkoa wa Mbeya waliopewa Computer mpakato yenye thamani ya Milion mbili (Tsh 2,000,000/-).

Umoja wa vijana CCM mkoa wa Mbeya waliopewa Pikipiki moja yenye thamani ya shilingi Milion mbili na laki mbili (Tsh 2,200,000/-), Murua Group wamepewa Milion mbili (Tsh 2,000,000/-) pamoja na Umoja wa Machifu Igawilo waliopewa jumla ya shilingi Milion moja (Tsh 1,000,000/-) ambapo jumla ya Shilingi Milion kumi na mbili na laki mbili zimetolewa zimetolewa na taasisi hiyo ili kuwawezesha kuendesha shughuli zao kwa ufanisi.

Katika hotuba yake Dkt. Tulia amesema “Kama mnavyofahamu kwamba mimi sio Mbunge wa sehemu moja hivyo basi hata kwenye Wilaya nyingine huko tumekwishafanya wote kazi na tutaendelea kufanya kazi kwa pamoja ili kuimarisha chama chetu lakini kwa leo wenyeji wetu walikuwa ni Mbeya jiji na lazima jumuiya zetu zifanye kazi vizuri na kwa ufanisi.”
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com