Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya
Kilimo, Mifugo na Maji,Mhe. Mahmoud Mgimwa,(katikati) akisalimiana na
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Mifugo (TALIRI) Tanzania
Dkt.Eligy Shirima upande wa kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na
Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel.
Kaimu Mtendaji Mkuu wa LITA chini
ya wizara ya mifugo Dkt.Pius Mwambene,akisoma taarifa kwa Kamati ya
Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ambayo ilitembelea Kituo cha Utafiti wa
Mifugo Mpwapwa(LITA) na Ranchi ya Taifa(NARCO),
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na
Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel, ,akizungumza katika ziara ya
kamati ya Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ambayo ilifanya ziara katika
Kituo cha Utafiti wa Mifugo Mpwapwa(LITA) na Ranchi ya Taifa(NARCO)
zilizopo mkoa wa Dodoma.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya
Kilimo, Mifugo na Maji,Mhe. Mahmoud Mgimwa,akizungumza na wataalamu
kutoka wizara ya mifugo wakati walipofanya ziara na kamati yake katika
Kituo cha Utafiti wa Mifugo Mpwapwa(LITA) na Ranchi ya Taifa(NARCO)
zilizopo mkoa wa Dodoma kushoto ni Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na Uvuvi
(Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel
Katibu Mkuu Wizara ya Mifugo na
Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel,akiwa kwenye maabara akitoa
maelezo kwa kamati Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ambayo ilifanya ziara
katika Kituo cha Utafiti wa Mifugo Mpwapwa(LITA) na Ranchi ya
Taifa(NARCO),zilizopo mkoani Dodoma
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya
Utafiti wa Mifugo (TALIRI) Tanzania Dkt.Eligy Shirima,akitoa maelezo kwa
kamati Bunge ya Kilimo, Mifugo na Maji ambayo ilifanya ziara katika
Kituo cha Utafiti wa Mifugo Mpwapwa(LITA) na Ranchi ya
Taifa(NARCO),zilizopo mkoani Dodoma.
………………………..
Na Alex Sonna,Mpwapwa
KAMATI ya Bunge ya Kilimo, Mifugo
na Maji imetembelea Kituo cha Utafiti wa Mifugo Mpwapwa(LITA) na Ranchi
ya Taifa(NARCO), huku ikishauri serikali kutoa fedha za kutosha kwa
ajili ya tafiti ili ziwe na tija kwa Taifa.
Kamati hiyo imefanya ziara yake
leo ikiambatana na Wataalam kutoka Wizara ya Mifugo wakiongozwa na
Katibu Mkuu wakikagua utendaji kazi wa kituo hicho na Ranchi ya Kongwa,
mkoani Dodoma.
Akizungumza katika ziara hiyo,
Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mahmoud Mgimwa, amesema kamati inapenda kuona
wizara inazoongoza ziingie na kuwa za kipaumbele kwa kuwa malighafi za
viwanda asilimia 85 inapatikana sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi.
“Kama serikali inataka tufanikiwe
kwenye maeneo haya ifike wakati tujielekeze kwa nguvu, tuishawishi
serikali ione umuhimu wa hizi taasisi, Tanzania ni miongoni mwa nchi
zinazosifika kwa ufugaji wa ng’ombe wengi bara la Afrika sasa
tunafaidikaje na hiyo sifa,”amesema.
Amesema hakuna nchi yeyote Duniani
iliyoendelea kama haijawekeza vya kutosha kwenye utafiti hivyo
imeelekeza uboreshaji zaidi wa wataalamu na vifaa kwenye utafiti.
“Tukichelewa kuwekeza vya kutosha
tukawapa fursa watu wa kutoka nje kuwekeza tutafanya utafiti kwa matakwa
yao, COSTECH wametoa fedha kidogo, kwenye Baraza la Mawaziri kipindi
cha nyuma serikali ilisema lazima itenge asilimia moja kutoka kwenye
Bajeti kuu kwenda kwenye utafiti, je, ni kweli inatengwa kwasababu
inatakiwa kugawanywa kwenye kilimo na mifugo,”amesema.
Awali, Katibu Mkuu Wizara ya
Mifugo na Uvuvi (Mifugo) Prof. Elisante Ole Gabriel , ameahidi
kutekeleza ushauri uliotolewa na wabunge huku akiwahamasisha waendelee
kuwekeza kwenye ufugaji.
“Mtusaidie sana wabunge
kuhamasisha jamii, endeleeni kufuga sana tunatamani muwe na mashamba na
sisi tutakuwa tayari kutuma wataalam wetu wawasaidie,”amesema.
Amesema lengo la wizara hiyo ni
kuona mageuzi ya kisayansi yanafanyika katika sekta ya mifugo na kwamba
haiwezekani kufanya mageuzi bila tafiti za uhakika.
“Ndio maana tunafundisha ili kutoa
taaluma hizi ambapo kutoka LITA ambao wanatoa taaluma mbalimbali ili
kupata wabobezi wa kwenda kusaidia wafugaji wetu, tungependa tuhame
kutoka kwenye uchumi wa uzalishaji twende kwenye uchumi wa kitaaluma,
tunaamini hilo litasaidia sana,”amesema.
Amebainisha kuwa bila kuunganisha utaalam na utafiti mambo hayawezi kwenda vizuri.
Katibu huyo amesema Wizara imejipanga kuhakikisha mageuzi ya kisayansi ya mifugo yanafanikiwa.
0 comments:
Post a Comment