Na Lucas Raphael, Igunga
MWALIMU wa Shule ya Sekondari ya Kata ya Igurubi, Maganga Ngassa (35)
amefi kishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Igunga kwa tuhuma ya kufanya
mapenzi na mwanafunzi wa miaka 17 anayesoma shule ya sekondari kidato
cha nne, Kata ya Mwisi wilayani hapa.
Mwendesha Mashitaka wa Polisi Igunga, Elimajid Kweyamba alidai mbele
ya Hakimu Juhudi Mdonya, kwamba Julai 25, mwaka huu saa 9 alasiri katika
nyumba ya kulala wageni ijulikanayo kwa jina la Forest au Chacha
iliyoko Mtaa wa Mwayunge mjini Igunga, kinyume na sheria za nchi, Ngassa
alifanya mapenzi na mwanafunzi wa mwenye umri wa miaka 17 anayesoma
shule ya sekondari iliyoko Kata ya Mwisi kidato cha nne (jina
linahifadhiwa). Mshitakiwa alikana kutenda kosa hilo ambapo kesi hiyo
imeahirishwa hadi Agosti 18, mwaka huu itakapotajwa tena.
Sunday, August 6, 2017
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
KARIBU TUME YA MAENDELEO YA USHIRIKA
Popular Posts
-
Kiongozi wa upinzani, Kizza Besigye akisindikizwa na maofisa wa gereza la Luzira alikokuwa akishikiliwa Kiongozi w...
-
Katibu Mkuu wa Wizara ya kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma Katibu Mkuu wa Wizara ya kilim...
-
📌 Asema Rais, Dkt. Samia anafanya kazi kubwa ya kuwaunganisha Watanzaia 📌 Atak...
-
Na Hamis Hussein - Singida Serikali imetoa shilling bilioni 5.9 kwaajili ya kuendeleza ujenzi wa majengo mapya ya hospitali ya rufaa y...
-
Na Debora Charles Kiyuga ✍🏽 Ni dhahiri kuwa mafanikio ya Uongozi Bora wa Mhe. Rais Daktari John Pombe Joseph Magufuli yamekuwa yak...
Powered by Blogger.

0 comments:
Post a Comment