METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, July 7, 2017

BOYS SAYARI KUBWA WAPOKELEWA KWA VISHINDO PEMBA

Na Mwandishi wetu kutoka Zanzibar

Jangombe Boys asubuhi ya leo imeondoka Unguja na kuelekea kisiwani Pemba kwa lengo la kuchukuwa point sita kwenye mechi mbili.

Timu imefika salama na imepokelewa kizalendo na wapezi wa Boys Pamoja na viongozi wa Friends of Boys waliotangulia wiki kabla kwa lengo la kwenda kuandaa mazingira mazuri ya makazi kula na eneo la kufanyia mazoezi muda wote wa siku nane ambao timu inakuwa Pemba alisema Alawi H. Foum Katibu wa Friends of Boys.

Alawi aliongeza kwa kusema viongozi waliotanguliwa wamefanikisha maandalizi yote na timu itaishi Pemba bila ya usumbufu timu iko Piki tunafarajika kupata mapokezi ya nguvu kutoka bandarini hadi tunaingia Piki imani yetu malengo yetu ya Kurudi na point sita yatatimia na jioni ya leo timu imefanya mazoezi mepesi katika kiwanja cha Jambieni kujiaandaa na mchezo wa awali zidi ya Mwenge na ule wa pili zidi ya Okapi

Alawi alipoulizwa juu ya wachezaji waliosafiri kama wapo fiti alisema wachezaji wako sawa hasa waliosafiri ukiachilia mbali wachezaji watatu ambao wamesafiri na combain ya wilaya ya mjini iliyokwenda Arusha kushiriki mashindano ya Rolling stone na Abdi kassim Babi atawasili Pemba kesho baada ya kuweka sawa mambo yake ya familia

Friends Of Boys imejipanga na ahadi zake zipo pale pale tuwaombe wapezi na wadau wote wa Boys waiombee timu irudi na point sita kwa kushinda mechi zote zidi ya Mwenge na Okapi ili timu ijiweke sehemu nzuri ya kufikia malengo yake ya kuchukuwa ubingwa.

Wadau wa Boys wakiipokea timu yao Kijijini Piki
Wachezaji wa Boys wakiwa mazoezi kisiwani Pemba uwanja wa Piki
Wadau wa Boys wakisindikiza timu yao kutoka bandarini kuelekea Piki
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com