METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, April 18, 2017

RC MASENZA AMTAKA MTENDAJI ALIYEPUUZA AGIZO LA MAKAMU WA RAIS KUJIPELEKA POLISI

Wananchi   wa Ipogolo  wakitoa malalamiko yao

Mwananchi akitoa malalamiko yake
Badhi ya  wananchi  waliotakiwa kuondoka
r />

Mkuu  wa  mkoa wa Iringa Amina Masenza  kushoto akimsikiliza mkuu wa  wilaya ya  Iringa Richard Kasesela kulia akiwataka wananchi kulinda  mazingira
Hivi  ndivyo  mazingira  yalivyoharibiwa mlima wa Ipogolo
kamati ya ulinzi na usalama mkoa wa Iringa ikiwa eneo la Ipogolo
Wananchi  wakimsikiliza mkuu wa  mkoa
Mkurugenzi wa Manispaa ya  Iringa kulia akiwa na mtendaji wa kata ya  kitanzini

Na MatukiodaimaBlog


MKUU  wa mkoa wa Iringa amemtaka  afisa mtendaji wa kata ya  Kitanzini katika Halmashauri ya wilaya ya  Iringa  kujisalimisha  kituo cha  polisi baada ya kukiuka agizo la makamu  wa Rais Samia Suluhu Hassan la utunzaji wa mazingira mlima wa Ipogolo.
 
Hatua  ya  mkuu  huyo wa  mkoa kuagiza mtendaji  huyo kuchukuliwa hatu kali imekuja baada ya kuruhusu wananchi wafanyabiashara ndogo ndogo  kuvamia msitu wa  hifadhi ya milima ya Ipogolo kwa  ajili ya ujenzi wa vibanda vya biashara kama  ambavyo jana  mtandao  wa matukiodaimaBlog  ulivyoibua taarifa  hii .
 
Akizungumza leo  eneo la soko la magari mabovu baada ya  kufanya  ziara  ya ghafla  eneo hilo  kushuhudia uharibifu  huo ,mkuu  huyo wa mkoa alisema  kuwa amesikitishwa na hatua ya  wafanyabiashara  hao kufyeka  miti ya asili kwa ajili ya ujenzi wa vibanda vya biashara .
 
Hivyo  alisema  kuwa hawezi  kukubali uharibifu huo wa mazingira kufanyika katika eneo hilo  na maeneo mengine ya mkoa wa  Iringa na kuwataka  wananchi kuturubuniwa na  watendaji kuingia maeneo ya hifadhi.
Alisema   kuwa Pamoja na  wafanyabiashara  wadogo wadogo  wa mashine tatu  kuhamishiwa  eneo la  soko la magari mabovu  ila  haina maana  kwao  kuvamia mlima na kuharibu mazingira kwa  kutaka  kujenga  vibanda  vya biashara .
 
“ Eneo  lililotengwa  kwa  ajili ya  wafanyabiashara  lipo  hivyo hakuna sababu ya kuharibu mazingira tumewatengea  eneo  la  kufanyia biashara  na isipo tosha hapa  ngome  kuna  soko ambalo hadi leo  halitumiki ipasavyo na   ni eneo kubwa kwa hili  namuagiza mtendaji wa kata  aliyehusika  kugawa mlima   huu afike  mwenyewe  polisi ili  achukuliwe hatua kali “
 
Aidha  mkuu  huyo wa mkoa ameagiza uongozi wa Halmashauri  ya Manispaa ya  Iringa  kusimamia  zoezi la  upandaji wa  miti katika  eneo  hilo ili  kurudisha hadhi ya mazingira  hayo .
 
Kwa  upande  wake  mkuu wa  wilaya ya  Iringa  Richard Kasesela  alisema  kuwa  atasimamia  agizo hilo la mkuu wa  mkoa na  kuwataja wananchi wanaoendelea  kujenga eneo hilo  kusitisha na kuwa mgambo  wa manispaa ya  Iringa  wataendelea  kulinda eneo  hilo .
 
Wakizungumzia  hatua  hiyo iliyochukuliwa na mkuu wa  mkoa wa Iringa  baadhi ya  wafanyabiashara  hao  walisema  kuwa mbli ya  mtendaji   huyo kuchukuliwa hatua bado anapaswa  kurejesha gharama zao   walizotumia kufanya maandalizi ya ujenzi  huo .
 
Kwani  walisema wao wasingefika kujenga  eneo hilo  bila kuelekezwa na  viongozi wa  serikali na kuwa ujenzi huo umeanza wiki  mbili kabla na serikali ya  Halmashauri ya  wilaya ilikuwa  ikiona  alisema Anitha Luhavi .
 
Wakati John Sanga alisema  kuwa  kabla ya  kupewa  eneo   hilo  walikuwa  wakitoa  pesa kwa  mtendaji  wa mtaa huo  ambae  alikuwa akiwapimia  eneo  na  kuwa  kila mmoja  alikuwa anapewa mita tatu za kujenga  kibanda japo  wapo  wengine  waliopewa  zaidi .
 
Hata   hivyo  afisa  mtendaji  wa kata ya  Kitanzini aligoma  kuzungumzia  suala   hilo  kwa madai  kuwa kwa sasa  ni  mtuhumiwa na  kulizungumzia na kwenda  kinyume na taratibu zake za kazi na atafika polisi kama  alivyotakiwa  ili  kutoa maelezo yake .
 
Mkurugenzi wa Halmashauri ya Manispaa ya  Iringa Dkt Wiliam Mafwere  alisema  kuwa wananchi hao  wamevamia  eneo  hilo  na hakuna ruhusa  ya uongozi  wa Halmashauri ya Manispaa kwa  wao kuvamia  hifadhi  hiyo ya  mlima Ipogolo .
 
Alisema  wanazingatia maagizo yote ya makamu  wa Rais  juu ya  uhifadhi wa mazingira na  kuwa  ni mara  kwa mara mkuu wa  mkoa wa Iringa anasisitiza juu ya  ulinzi na usimamizi wa hifadhi  za mazingira.
Akiwa  mkoani  Iringa siku  tano  zilizopita makamu wa Rais  Samia Suluhu  Hassan  aliagiza  viongozi wa  mkoa wa Iringa  kutunza mazingira na kuzuia  wananchi kulima ama   kujenga  katika hifadhi za  milima kwa ajili ya kuhifadhi ikolojia yam to Ruaha  mkuu ambayo  imetoweka kutokana na uharibifu wa mazingira unaofanywa na  wananchi  huku  mto  huo ukitegemewa na watu zaidi ya  milioni 8 pia Taifa  kwa ujumla  kutokana na uzalishaji wa umeme wa bwawa la Mtera na  Kidato .
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com