METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, March 23, 2017

Watu wanne wauawa nje ya jengo la Bunge la Uingereza

media
Idara mbalimbali za dharura wako kwenye daraja la Westminster mjini London, baada ya shambulizi la tarehe 22 Machi, 2017.

Watu wnne ikiwa ni pamoja na mshambuliaji na polisi, wamepoteza maisha kwenye daraja la Westminster katikati mwa mji wa London kufuatia milio ya risasi iliyosikia mapema siku ya Jumatano mchana karibu na jengo la Bunge la Westminster. Polisi inachukulia tukio hilo kama shambulizi la kigaidi.

Kwa mujibu wa mashahidi, kulisikika angalau risasi nne. Polisi waliotumwa katika eneo la tukio wamesema kuwa kuna mtu mmoja ambaye alipigwa risasi.

Kwa mujibu wa chanzo cha usalama watu wengi wamejeruhiwa, ikiwa ni pamoja na wanafunzi watatu, raia wa Ufaransa. Tukio hilo lilitokea nje ya jengo la Bunge, karibu na daraja katika ya eneo hilo ambapo basi pia iliwajeruhi wapita njia.

Polisi akitoa ulinzi nje ya nje ya jengo la Bunge wakati wa milio ya risasi kwenye daraja la Westminstermjini London, nchini Uingereza Machi 22, 2017.

Kwa mujibu wa msemaji, Waziri Mkuu wa Uingereza Theresa May "anaendelea vizuri".

Bi May alizungumza mbele ya wabunge mapema mchana lakini msemaji wake amekataa kuthibitisha kama alikua katika jengo la Bunge la Westminster au karibu na jengo hilo wakati wa shambulio.
Idadi ya hatua za usalama zimechukuliwa na mamlaka ambayo imesitisha matembezi na utalii.BBC
Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com