METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, November 1, 2016

Rwanda: maofisa waandamizi 22 wa Ufaransa walihusika katika mauaji ya kimbari

media
Rais wa Rwanda Paul Kagame akiwasha moto wa kumbukumbu katika eneo la kumbukumbu la mauaji ya kimbari mjini Kigali, wakati wa maadhimisho ya miaka 21 ya mauaji ya kimbari, Aprili 7, 2015.

Tume ya Kitaifa dhidi ya Mauaji ya Kimbari nchini Rwanda imetoa orodha ya maafisa waandamizi 22 wa Ufaransa ambao inawatuhumu kuhusika katika mauaji ya kimbari ya mwaka 1994, katika kukabiliana na uamuzi wa majaji wawili wa Ufaransa wanaoendesha upya uchunguzi katika shambulio dhidi ya ndege ya Rais wa zamani Juvenal Habyarimana.

"Maafisa wa ngazi ya juu wa Ufaransa na wanasiasa walitekeleza uhalifu mbaya nchini Rwanda," Tume ya Kitaifa dhidi ya Mauaji ya Kimbari (CNLG) imeshtumu katika ripoti iliyowasilishwa Jumanne kwenye ofisi za shirika la habari la AFP. Ripoti hii inayojulikana kamai "njama ya kesi ya ndege ya Habyarimana, Ufaransa yahusika katika mauaji hayo. "

Rwanda inaishtumu kwa miaka ukadhaa Ufaransa kushiriki katika mauaji ya kimbari, ambapo watu zaidi ya 800,000, wengi wao wakiwa kutoka jamii ya Watutsi waliuawa. Shambulizi la Aprili 6, 1994 dhidi ya ndege ya rais, ambapo aliuawa rais wa kutoka jamii ya Wahutu Juvenal Habyarimana na mwenzake wa Burundi Cyprien Ntaryamira, linachukuliwa kama tukio lililozua mauaji ya kimbari.

Lakini uhusiano kati ya nchi hizi mbili uliingia upya matatani tangu mahakama ya Ufaransa kuanzisha uchunguzikwa kusikia ushuhuda wa mkuu wa zamani wa majeshi ya Rwanda, Kayumba Nyamwasa, ambaye anamtuhumu Rais wa sasa wa Rwanda, Paul Kagame, kwamba ndiye mwanzilishi wa shambulizi dhidi ya rais Juvenal Habyarimana.

Kwa mujibu Tume ya Kitaifa ya Kupambana dhidi ya Mauaji ya Kimbari (CNLG), uamuzi wa hivi karibuni wa Uifaransa kuanzisha upya uchunguzi kuhusu shambulio dhidi ya ndege ya rais Juvenal Habyarimana Aprili 6, 1994 "inalenga kuficha" ukweli kuhusu kuhusika kwa Ufaransa katika mauaji ya kimbari nchini Rwanda. Tume hii imetoa orodha ya maafisa wandamizi 22 wa Ufaransa ambao wanatuhumiwa kula njama bali pia kwa kuhusika katika mauaji hayo. "Maafisa wa Ufaransa walihusika katika mauaji ya kimbari kama wahalifu na washirika," CNLG imebaini.

Jenerali Jacques Lanxade, aliyekuwa Mkuu wa majeshi ya Ufaransa, na jenerali Jean-Claude Lafourcade, ambaye alikua kiongozi wa kikosi kiliyojulikana kwa jina la Turquoise Juni 22, 1994 nchini Rwanda chini ya mamlaka ya Umoja wa Mataifa ni miongoni mwa maafisa hao waandamizi 22 wanaotajwa kuwa walihusika katika mauaji ya kimbari yaliyotokea nchini Rwanda mwaka 1994.

Nchini Rwanda, kamati ya uchunguzi ilibaini kwamba shambulizi dhidi ya ndege ya Rais Habyarimana lilitekelezwa na watu wenye msimamo mkali kutoka jamii ya Wahutu kutaka kumuangamiza rais ambaye waliona kuwa ni mwenye msimamo wa wastani.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com