METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, September 20, 2016

PROFESA JUMANNE MAGHEMBE AKABIDHI ENEO LA HEKALI 50 KWA WANAKIJIJI MKURANGA MKOANI PWANI


 WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe (kulia) akisalimiana na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, baada ya kuwasili katika kijiji cha Kipara Mpakani kwa ajili ya kukabidhi eneo la hekali 50 kwa wanakijiji hicho, Mkuranga, mkoani Pwani.

 WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, akisaini kitabu cha wageni kabla ya mkutano na wanakijiji cha Kipara Mpakani. Kushoto ni Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega.

 Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, akihutubia wanakijiji cha Kipara Mpakani kabla Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Maghembe kukabidhi eneo la hekali 50 kwa kijiji hicho kwa ajili ya huduma za kijamii.

 WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe, akihutubia wanakijiji katika mkutano huo kabla ya makabidhiano.

 MZEE wa Kijiji cha Kipara Mpakani akimshukuru Waziri wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, kwaniaba ya wanakijiji hicho.

 WANAKIJIJI wakimpengeza Mbunge wao, Ulega baada kufanikiwa kupewa eneo hilo la hekali 50.

WAZIRI wa Maliasili na Utalii, Profesa Jumanne Maghembe (kushoto) na Mbunge wa Mkuranga, Abdallah Ulega, wakikata majani kuashiria kukabidhi rasmi eneo hilo kwa ajili ya huduma za kijamii.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com