Askari polisi wakipiga doria katika mtaa wa mji wa Bujumbura, Aprili 12, 2016.
Wachunguzi
huru wa Umoja wa Mataifa wametoa orodha ya watuhumiwa ambao wanapaswa
kufunguliwa mashitaka kwa uhalifu dhidi ya ubinadamu ambao inawezekana
kuwa ulitekelezwa nchini humo.
Uchaguzi
wa Pierre Nkurunziza kwa mara nyingine mwezi Julai 2015 haukubadili
chochote. Watu wanaendelea kuuawa na wengine kupotezwa, Idara ya
Ujasusi, vikosi vua ulinzi na polisi vinanyooshewa kidole na upande
mwengine makundi ya watu wenye silaha.
Visa vya kukamatwa kiholela na mateso
Wachunguzi
huru wa Umoja wa Mataifa wamehitimisha kuwa ni vigumu kujua kiwango
kamili ca uhalifu uliofanywa, "lakini tuna orodha ya maafisa waliohusika
na visa hivi, " Christof Heyns alioshiriki katika uchunguzi huo
amesema, akinukuliwa na Deutsche Welle. Wachunguzi wanasema kuwa
wamekusanya ushahidi wa ubakaji, mauaji, kutoweka kwa watu, kukamatwa na
kuteswa. Umoja wa Mataifa umeorodhesha watu 564 waliouawa nchini
Burundi tangu mwezi Aprili 2015. Afisa mwandamizi wa zamani wa jeshi
amewambia wachunguzi kwamba kuna orodha ya watu wanaotafutwa ili wauawe.
Ushahidi tosha
Mashahidi
wamewataja maafisa 12 wa ngazi ya juu katika vikosi vya usalama ambao
wamekua wakitoa taarifa moja kwa moja kwa serikali kama wanahusika na
visa vya kutoweka kwa watu katika mazingira tatanishi.
0 comments:
Post a Comment