Madhara ya vita Syria
Marekani
imesema ndege za kivita za Urusi zinahusika kushambulia msafara wa
misaada nchini Syria siku ya Jumatatu na kusababisdha vifo.
Maafisa
wa Marekani wameiambia BBC ndege mbili za kivita za Urusi aina ya SU-24,
zilikuwa angani, sambamba na msafara huo wa magari, wakati tukio hilo
likitokea.
Hata hivyo Urusi imekana na kusema kuwa ndege hizo hazikuwa zake wala za Syria, na kutupia lawama wapiganaji wa waasi.
Wizara ya
Ulinzi ya Urusi imesema ndege zake zinazojiendesha zenyewe zilikuwa
zikifuatilia msafara huo, lakini kamera zao zilijizima kabla ya
mashambulizi kuanza.
Shambulio hilo la Jumatatu lilifanyika saa kadhaa baada ya serikali ya Syria kutangaza kumaliza wiki ya kusitisha mapigano. BBC
0 comments:
Post a Comment