METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, December 22, 2015

Kagame Ampa tano Magufuri....






RAIS Paul Kagame wa Rwanda amefurahishwa na hatua ambazo Rais John Magufuli anazichukua, hasa katika usimamizi na utendaji kazi wa bandari huku akimhakikishia kuwa Rwanda iko tayari kushirikiana na Tanzania, hasa katika kuitumia Bandari ya Dar es Salaam.

Siku chache baada ya kuingia madarakani, Rais Magufuli akimtumia Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, alifanya ziara ya ghafla katika Bandari ya Dar es Salaam, ambako alifichua ufisadi wa mabilioni ya shilingi kutokana na upotevu wa makontena, ambayuo hayakulipiwa kodi stahili kwa serikali.
 
Kutokana na ufisadi huo, Rais aliivunja Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari (TPA), alitengua uteuzi wa Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Awadhi Massawe na kusimamisha maofisa kadhaa wa bandari hiyo na wengine wanaohusika na usimamizi wa bandari kavu.
 
Aidha, alimsimamisha kazi Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Rished Bade na maofisa wengine wa mamlaka hiyo, ambao miongoni mwao tayari wamepandishwa kizimbani katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam kutokana na ubadhirifu huo.
 
Kutokana na hilo, Rais Kagame kupitia kwa Balozi wake nchini, Uegene Kayihura, amempongeza Rais Magufuli kwa hatua alizochukua kusafisha uozo katika bandari hiyo, ambayo Rwanda inapitisha asilimia 70 ya mizigo yake. Dk Magufuli jana alikutana na kufanya mazungumzo na Balozi Kayihura Ikulu jijini Dar es Salaam.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com