Dodoma, Tanzania - Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Mussa Azzan Zungu (Mb), ametangaza kwa masikitiko makubwa kifo cha Mbunge wa Peramiho, Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama, kilichotokea tarehe 11 Desemba, 2025 Jijini Dodoma.
Katika taarifa yake, Spika Zungu ametoa pole kwa Waheshimiwa Wabunge wote, familia ya marehemu, ndugu, jamaa pamoja na Wananchi wa Jimbo la Peramiho. Ameeleza kuwa ni kipindi kigumu kwa wote waliomfahamu na kushirikiana na marehemu, na amewaombea moyo wa uvumilivu na subira.
“Kwa masikitiko makubwa, naomba kutangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho Mheshimiwa Jenista Joakim Mhagama kilichotokea leo 11 Desemba, 2025 Jijini Dodoma. Natoa pole kwa Waheshimiwa Wabunge wote, familia ya Marehemu, ndugu, jamaa na Wananchi wa Jimbo la Peramiho, Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu,” amesema Spika Zungu


0 comments:
Post a Comment