METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, February 8, 2024

SERIKALI YAOMBWA KUAJIRI WALIMU ILI KUENDANA NA IDADI KUBWA YA WANAFUNZI- MBUNGE KAKONKO KAMAMBA.




Na Saida Issa, Dodoma

MBUNGE wa Buyungu kakonko Alloyce Kamamba amesema kuwa Serikali imefanya vizuri katika ujenzi wa shule za sekondari na msingi kwa kujenga madarasa,vyoo pamoja na nyumba za walimu hali iliyopelekea idadi ya wanafunzi kuongezeka huku akiomba Serikali kuajiri walimu ili kuwapunguzia mzigo wa majukumu. 

Hayo ameyaeleza Bungeni Jijini Dodoma alipokuwa akitoa maoni yake kwa kamati ya kudumu ya Bunge,ustawi na Maendeleo ya jamii. 

Alisema kuwa ongezeko la wanafunzi halikuenda sambamba na ongezeko la kuajiri walimu alisema kuwa Kwa upande wa elimu ya sekondari uhitaji wa walimu ni kwa asilimia 47 na upande wa shule za msingi uhitaji wa walimu ni asilimia 42.

Akizungumzia Mkoa wa Kigoma alisema kuwa uhitaji wa walimu sekondari no asilimia 33 upande wa shule za msingi ni asilimia 46.

"Nikichukua wilaya yangu ya kakonko uhitaji wa walimu shule za msingi ni asilimia 38 na upande wa sekondari ni asilimia 52,ukiangalia kwa jumla bado walimu waliopo na wanaohitajika ni nusu kwa nusu,

Ninachoshangaa mheshimiwa mwenyekiti ni kuona kwamba walimu wapo kwa asilimia 47 lakini wanafaulisha kwa asilimia 80 maana yake mini mheshimiwa mwenyekiti walimu wa Nchi hii wamefanya kazi ya ziada kuziba lengo la walimu ambao hawapo,hoja yangu mwenyekiti walimu waajiriwe,"alisema.

Pia aliiomba Serikali kujenga mabweni katika shule za kata ili kuwapunguzia changamoto ya jua pamoja na mvua mwanafunzi.

Alisema kuwa kuwepo kwa mabweni kutasaidia kuwa na uhakika na makazi ya mwanafunzi pindi wawapo shule pia walimu kuweza kuwafatilia wanafunzi hao.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com