METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, February 16, 2024

MBUNGE OLE LEKAITA AKABIDHI MAGARI MAWILI YA WAGONJWA KITUO CHA AFYA SUNYA-KITETO

Na Mathias Canal, Kiteto-Manyara

Kituo cha afya cha Sunya kilichopo katika Wilaya ya Kiteto kimekabidhiwa magari mawili ya wagonjwa (Ambulance) kwa ajili ya kuwahudumia wananchi.

Akizungumza mara baada ya kukabidhi magari hayo jana tarehe 16 Februari 2024 Mbunge wa jimbo la Kiteto mkoani Manyara Mhe Edward Ole Lekaita amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt Samia Suluhu Hassan ametoa magari hayo ili kupunguza adha wanazozipata wananchi.

Amesema Rais Samia ametoa magari matatu ambapo mawili kati ya hayo yamewasili mjini Kiteto, magari mawili yatakuwa kwaajili ya wagonjwa na moja kwaajilia ya madaktari.

Mbunge Ole Lekaita amewataka wahudumu wa afya pamoja na wananchi wote kuhakikisha wanayatunza magari hayo ili yaweze kutumika kuwahudumia kama serikali ilivyokusudia.

Hafla hiyo ilihudhuriwa pia na Mbunge wa Jimbo la Msalala Mhe Iddy Kassim pamoja na Mbunge wa Jimbo la Moshi Mjini Mhe Priscus Tarimo ambao kwa pamoja wamempongeza Mbunge huyo kwa kazi kubwa na nzuri wanayoifanya ya kuwatumikia wananchi kwa ufasaha.

Wamewasihi wananchi kuendelea kumuunga mkono na kumuombea mbunge wao ili aendelee kutekeleza majukumu yake ipasavyo.

MWISHO
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com