METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, April 7, 2023

TANESCO YATOA FUTARI KWA WENYE UHITAJI SINGIDA // SHEIKH ISSA NASSORO ATOA PONGEZI NA KUZITAKA TAASISI ZINGINE KUIGA UTARATIBU KAMA WA SHIRIKA HILO

 










Na Hamis Hussein - Singida

SHIRIKA la Umeme Tanzania TANESCO kwa Mkoa wa Singida Limetoa Sadaka ya Futari yenye thamani ya Shilingi Laki sita kwa Wajane, Yatima, Wazee na watu wengine wenye mahitaji maalum ikiwa ni sehemu yake ya kurejesha kwa jamii.

Hafla hiyo imefanyika Jana April 6, 2023 katika Msikiti wa Taqwa Mjini Singida kupitia Kitengo cha kusaidia jamii yenye uhutaji ya Nusrat Al Ummati iliyochini ya ofisi ya Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Singida ikiambatana na ugawaji wa Tende kutoka kwa Mkurugenzi wa Tabligh na Da’awa.

Akizungumza kwa niaba ya Meneja wa TANESCO Mkoa wa Singida Afisa Usafirishaji Juma Ally Omary amesema shirika hilo limeitikia wito wa ofisi ya Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Singida ambayo ulilitaka shirika hilo kuwasaidia kundi watu wenye mahitaji maalum.

“Leo tuko kwenye jambo mhimu jambo la kuwasaidia wenye uhitaji Sheikh alitufikishia sisi barua Tanesco Mkoa wa Singida na kwa vile taasisi yetu inashughulika na kuhudumia jamii na inabidi irudishe kwa jamii na sisi tukaona ndani ya muda huu mchache tuungane na wenzetu katika mwezi huu wa Ramadhani” alisema Omary

Afisa huyo ameongeza kwa kulipongeza baraza la Waislamu Tanzania Bakwata kwa kuwa kiunganishi na Jamii hivyo Tanesco inaunga jitihada za Mufti na Sheikh Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Bin Zuberi ya kuwasaidia wenye uhataji.

Kwa upande wake Afisa Uhusino na Huduma kwa wateja Bi Rehema Mwaipopo alisema kuwa Shirika  hilo la Umeme linaihudumia Jamii hivyo limeungana na watu wenye uhitaji katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ambapo aliongeza kwa kuiomba ofisi ya Sheikh wa Mkoa kuliombea shirika hilo ili liendelee kuwahudumia wananchi.

Naye Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Singida Sheikh Issa Nassor amelishukuru shirika la umeme Tanzania kwa Mkoa wa Singida  kwa kuwaajali wenye uhitaji ambapo ametumia nafasi hiyo kuyataka mashirika na taasisi zingine kuiga mfano kutoka Tanesco wa kusaidia jamii badala ya kusubiri wadau kutoka nje ya nchi

Sheikh Nassoro alisema kuwa wajane na Yatima ni watu wa karibu na jamii kwa historia ya ukoo na dini pamoja na utanzania ambapo aliwataka wadau wengine kusaidia jamii

“ Nawashukuru sana Tanesco Mkoa wa Singida kwa kuwajali wenye uhitaji na nitowe wito kwa mashirika mengine kama vile viwanda vya mafuta, na taasisi zingine kuiga mfano wa TANESCO kwa kuwasaidia wajane, Watoto yatima, wafungwa wa magereza ni aibu yaani hadi waje watu kutoka Uturuki na Misri  kuwasaidia ndugu zetu” . Alisema Sheikh Issa Nassoro.

Hata hivyo Mwenyekiti wa Kitengo cha Kusaidia jamii yenye Uhitaji kama vile Wajane, Yatima na Wazee ambao hawajiwezi cha Nusrati Al Ummati Ally Amani aliishukuru TANESCO Mkoa wa Singida kwa kutoa Futari hiyo pamoja na Taasisi ya Sheikh Arfu ambayo imetoa Tende.

“Mashallah wapendwa kaka zetu, Wapendwa shirika letu la Tanesco tunashukuru sana kwa msaada mlitofanyia na tunawaombe mwenyezi Mungu awafanyie wepesi na kuwatimilizia mahitaji yenu karibuni tena kwenye ofisi ya sheikh Mkuu wa Mkoa wa Singida. Vilevile tunamshukuru sheikh Arfu na kampuni yake kwa kutulelea tende kama boksi 20  tunamshukuru sana na tunamuomba  allah amsamehe makosa yake  kheri ya mwenyezi Mungu ziwe juu yake” . Alisema Amani

 

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com