Aliyekuwa Katibu Tawala Mkoa wa Singida ambaye amestaafu Mwl Dorothy Mwaluko(Kulia) akimkabidhi Nyaraka Katibu Tawala Mpya Dkt Fatma Mganga mapemba leo Machi 21, 2023. |
Katibu Tawala Mpya wa Mkoa wa Singida Akizungumza na watumishi wa Mkoa wa Singida |
Watumishi wa Mkoa wa Singida wakifuatilia Hafla ya makabidhiano ya ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida. |
Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba Akizungumza kwenye hafla hiyo. |
Issa Nassor Sheikh Mkuu wa Mkoa wa Singida Akizungumza kabla ya kusoma dua wakati wa makabidhiano ya ofisi ya Katibu Tawala wa Mkoa wa Singida. |
Makabidhiano yakiendelea. |
Na Hamis Hussein - Singida
KATIBU Tawala wa Mkoa wa Singida Dkt. Fatma Mganga amewataka
watumishi wote mkoani hapa kutoa ushirikiano na kuacha majungu na kwamba
hatamvumilia mtumishi yeyote atakayekuwa na majungu mahala pa kazi.
Dkt. Mganga amesema hayo leo Machi 21, 2023 wakati akizungumza na watumishi na wakuu wa idara
wa Mkoa wa Singida baada ya kukabidhiwa
ofisi na aliyekuwa Katibu Tawala mkoani hapa ambaye amestaafu Mwl. Dorothy.
Dkt. Mganga ambaye awali alikuwa katibu tawala Mkoa wa Dodoma amesema Majungu kwa watumishi wa umma mahala pakazi yanasababisha migongano na kupelekea kukwamisha utendaji na kushindwa kutimiza malengo hivyo akasisitiza kuwepo kwa ushikiano katika kutimiza malengo ya serikali ya kuwahudumia wananchi.
“Mimi nitakuwa tayari kupokea maoni lakini sitakuwa tayari kupokea majungu, sidhani kama ukija ukaniambia ‘unajua Grace kazi yake ni hivi, yule hafai hata kidogo’ mimi nitakuuliza je wewe na yeye mkoje? Ili ukamilishe hadithi nzima, kwa sababu majungu mahala pakazi huwa yanaleta migongano na mwisho wa siku huwa tunashindwa kufikia malengo ambayo tumeelekezwa kwahiyo sitapenda majungu lakini nakaribisha maoni” alisema Dkt Mganga.
RAS Dkt Mganga aliongeza kwa kuwataka watumishi hao kushirikiana
katika kuwatumikia wananchi ambao ndio wanafanya wawepo katika nafasi
walizonazo badala ya kuwaona wanawapotezea muda.
“Mimi pekee yangu sitaweza
lakini tukishirkiane kwa pamoja ninaamini tutakwenda kufanya mambo makubwa
katika Mkoa wa Singida,Dorothy alifanya vizuri sana na mimi ninaomba ushirikiano
ili tukaboreshe pale ambapo Dorothy alisukumba basi sisi tuliobakia tuendelee
tokea pale, Lakini niwaombe kutenda kazi kwa bidii, wananchi ndio waajiri wetu
twendeni tukawatumikie watu wa Singida tusiwaone kama wanatupotezea muda” Aliongeza Dkt Mganga.
Kwa Upande wake Mkuu wa Mkoa wa Singida Peter Serukamba alimshukuru
Katibu Tawala ambaye amestaaafu Mwl. Dorothy
Mwaluko katika utendaji wake ambapo pamoja na mambo mengine alifanikisha
maendeleo mengi katika nyaja mbalimbali za Mkoa huu hivyo akatumia nafasi hiyo
kumshukuru kwa utumishi wake na kwamba
alimrahisishia utendaji wake kazi wa
Ukuu wa Mkoa.
RC Serukamba aliongeza kwa kuwataka watumishi wa Mkoa wa
Singida kutekeleza majukumu yao ikiwa ni pamoja kufatilia na kuielelewa miradi
inayotekelezwa hasa ngazi za hamalshauri ambapo amewaonya baadhi ya watumishi hao kuwa waongo pindi wanapoulizwa kuhusu mambo wanayoyasimamia.
“Kwenye halmashuri kugumu
bado watu wanacapacity ya kusema uongo, mtu wa halmashauri ukimuliza jambo jibu
jiulize mara mbili, kuna chance anakudanganya lakini sasa tumepata RAS
aliyeanzia kwenye halmashauri hivyo
anawajua, kwahiyo uongo mliokuwa mnaniambia mimi msipeleke huko maisha yenu
yatakuwa magumu sana, wengi wenu hamfanyi kazi kwa bidii, nyie mnatuma na
yule mliomtuma naye anatuma matokea yake vitu vinakuwa haviko kwenye mikono yenu kwahiyo ni rahisi watu wote tukawa tumedanganywa”
Alisema RC Serukamba.
Naye aliyekuwa Katibu Tawala Mkoa wa Singida ambaye
amestaafu Mwl. Dorothy Mwaluko amewashukuru watumishi wote wa Mkoa wa Singida
kwa ushirikiano wao katika mambo mbalimbali ya kiutendaji ambayo yameleta
chachu ya maendeleo kwa wananchi huku akiwataka watumishi hao kuendelea kuwatumika
wananchi wa mkoa wa Singida ili kutimiza
malengo yaliyowekwa na Serikali.
Mwl. Mwaluko alisisitiza watumishi kuwajibika katika utatuzi
wa changamoto za wananchi wa Singida ambapo amesema utashi wao katika kutumikia
wananchi kwa kufuata taratibu za utumishi wa umma utasaidia katika kutimiza
malengo ya serikali ya kutatua changamoto za wananchi.
0 comments:
Post a Comment