METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, June 19, 2022

WANAFUNZI WA KIISLAMU WAOMBWA KUTUMIA ELIMU ZAO KUISAIDIA JAMII





Naibu amir wa Taasisi ya JAI DODOMA ENG. SALEHE JUMA amewataka wanafunzi wa kiislamu wanaomaliza masomo yao kwenda kuyaishi yale mambo mema waliyojifunza katika jamii na kujitoa katika masuala mbalimbali ya Dini ili kuupeleka uislamu mbele na elimu zao kuwa na tija chanya katika jamii.

ENG. SALEHE JUMA ametoa wito huo katika mahafali ya jumuiya ya wanafunzi wa kiislamu wa chuo cha serikali za mitaa Hombolo mkoani Dodoma ambapo amewasisitiza wahitimu hao kwenda kutumia elimu yao katika kutoa msaada katika jamii ili elimu yao iwe na tija chanya kwa jamii.

Aidha ENG. SALEHE JUMA akatumia fursa hiyo kueleza historia ya Taasisi ya JAI pamoja na kazi zinafanywa na JAI ikiwemo kusaidia watu wasojiweza, kuhudumia wagonjwa chakula, kuzika watu ambao hawana ndug pamoja na kuchangia Damu ili kuokoa maisha ya watu.

Katika hatua nyingine ENG. SALEHE JUMA kwa niaba ya Taasisi ya JAI DODOMA akaadidi Taasisi ya JAI DODOMA kuisaidia jumuiya ya wanafunzi wa kiislamu chuo cha Hombolo mazulia (mikeka) kwaajili ya kufanyia ibada ili kuwawezesha wanafunzi wa chuo hicho kuteleza ibada kwa urahisi.

Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com