METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, April 16, 2022

JESHI LA POLISI SINGIDA LAMKAMATA MWIZI WA DIZELI LITA 300 NA WAFANYABIASHARA WA BANGI // LATOA TAHADHARI KUELEKEA SIKUKUU YA PASAKA

 


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Singida ACP Stella Mutabihirwa akionyesha misokoto bangi Iliyokamatwa na jeshi la polisi katika Msako wa April 10 na 12 mwaka huu.


Misokoto ya bangi iliyokamatwa kwa mwanamke  mfanyabiashara wa madawa hayo mkoani singida 

Kamanda wa polisi mkoa wa Singida ACP Stella Mutabihirwa akiwaonyesha waandishi wa habari misokoto ya bangi

ACP Stella Mutabihirwa akiaangalia misokoto ya bangi  wakati akitoa taarifa kwa waandishi wa habari baada ya kuwakamata wahalifu wanajihusisha na biashara hiyo.


Madumu ya mafuta  ya Dizeli lita 300 aliyokuwa akiyaiba kwenye magari makubwa yaliyokamatwa kwa mtuhumiwa ajulikanaye  kama Emanuel Juma (29) mkazi wa Ulyampiti wilaya yaIkungi  mkoani Singida.


Na Hamis Hussein - Singida

JESHI la Polisi Mkoani Singida Katika misako na oparesheni iliyofanya kuanzia april mosi hadi 16 mwaka huu limebaini matukio mbalimbali ya uhalifu ambayo ni wizi wa mafuta ya dizeli pamoja na umiliki wa misokoto ya bangi katika maeneo ya kadhaa ya mkooni hapa.

Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari kamanda wa polisi mkoa wa Singida ACP Stella Mutabihirwa amesema jeshi hilo linamshikilia mwanamke mmoja wa umri wa miaka 29  ambaye jina lake limehifadhiwa mkazi wa Mnung’una kata ya minga  wilaya ya Singida baada ya kukutwa na  bangi ambapo amekuwa akijihusisha na uuuzaji wa madawa hayo ya kulevya ambapo ameonekana kuwa akifanya biashara ya kuuuza bangi wa watu .

ACP Mutabihirwa alisema kuwa Mwanamke huyo alikuwa na misokoto 1948 ya bangi sawa na  kilogramu kumi na tayari  anashikiliwa  kwa uchunguzi zaidi ili kubaini mtandao mzima wa wauzaji wa madawa ya kulevya mkoani hapa .

“Tulifanikiwa kumkamata mwanamke mmoja siku ya tarehe 10 mwezi wa nne ambaye jina lake tumelihifadhi ni mwanamke mwenye umri wa miaka 29, alikamatwa katika maeneo ya Mnung’una kata ya Minga Wilaya ya Singida. Mwanamke huyu amekuwa akijihusisha na uuzaji wa bangi na alikutwa na misokoto ya bangi 1948 sawa na kilogram 10 alizokuwa amezihifdhi kwenye salfeti kwa lengo la kuisambaza na kuiuza katika mkoa wetu wa singida” . Alisema Kamanda ACP Mutabihirwa.

Kamanda ACP Stella Mutabihirwa aliongeza kuwa katika oparesheni ilifanyika april 12 jeshi hilo lilifanikiwa kumkamata mtuhumiwa mwingine aliyekutwa na misokoto 671 sawa na gramu 2 ambazo alikuwa amezihifadhi kwenye salfeti na na kwamba jeshi hilo bado linaendelea na msako kubaini mtandao mzima wa wasambazaji wa madawa ya kulevya ndani ya mkoa wa Singida.

Katika Msako wa jeshi hilo mnamo april 9 mwaka huu katika kijiji cha Ulyampiti  wilaya ya Ikungu liliweza kumkamata  mtuhumiwa mmoja aliyejulikana kwa jina la Emanuuel Juma  mwenye umri wa miaka 29  akiwa na mafuta ya Dizeli lita 300 ndani ya madumu 18 ya lita 20.

ACP Stella alisema mtuhumiwa huyo (Emanuel) alikuwa akiiba mafuta kwenye magari makubwa yapitayo Ikungi mkoani hapa kisha kuchukua mafuta na kuwauzia wananchi kutokana na kupanda kwa bei ya mafuta nchini na katika soko la dunia.

“Katika msako wa jeshi la polisi wa april 9 mwaka huu tulifanikiwa kumkamata mtuhumiwa wa wizi wa mafuta ya dizeli,Tulipata taarifa kuwa kuna mwananchi mmoja anafahamika kwa jina la Emanuel Juma mwenye umri wa miaka 29, anajihusisha na wizi wa mafuta ya Dizeli katika magari makubwa amabyo yanayopita hapo Ikungi kwahiyo aliweza kuhifadhi lita 300 za dizeli nyumbani kwake na kutokana na kupanda  kwa bei ya mafuta amekuwa akiwauzia watu kwa bei ya nchini”  alisemea ACP Mutabihirwa.

Kuhusu sikukuu ya Pasaka Kamanda Mutabihirwa aliwataka wakazi wa mkoa wa Singida kusherekea kwa amani  ambapo aliwataka wazazi na walezi kuhakikisha wanaacha watu majumbani ili kuwa walinzi wa miji yao pindi watakapokuwa katika nyumba za ibada pamoja na maeneo ya kusherekea na kuongeza kuwa jeshi hilo litaendelea na doria za miguu , magari pikipiki na doria za mbwa kama ulivyo utaratibu wao  ili kuhakikisha mkoa wa Singida unakuwa salama  wakati huu wa kusherekea sikukuu hiyo.

 

Share:

Related Posts:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © 2025 WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com