METDO Tanzania

METDO Tanzania

Monday, August 9, 2021

MWILI WA ALIYEKUWA WAZIRI WA ULINZI ULIVYOWASILI NYUMBANI KWAKE

Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga Dkt. Philemon Sengati akiongoza mamia ya waombolezaji waliofika katika Msiba wa aliyekuwa Waziri wa Wizara ya Ulinzi John Elias Kwandikwa Kijijini kwake Butibu Kata ya Kinamapula Halmashauri ya Ushetu Shinyanga. 

Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Wizara ya Ulinzi John Elias Kwandikwa uikisindikizwa na Makamanda wa JWTZ kutoka kwenye nyumba yake kuelekea eneo maalum kwajili ya kutoa nafasi kwa wana Ushetu kuaga mwili huo Kijijini kwake Butibu Kata ya Kinamapula Halmashauri ya Ushetu Shinyanga. 

Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Wizara ya Ulinzi John Elias Kwandikwa uikisindikizwa na Makamanda wa JWTZ kutoka kwenye gari maalum la Kijeshi ili kupelekwa nyumbani kwake kabla ya kuendelea na taratibu za kuaga mwili huo kijijini kwake Butibu Kata ya Kinamapula Halmashauri ya Ushetu Shinyanga. 

Mwili wa aliyekuwa Waziri wa Wizara ya Ulinzi John Elias Kwandikwa ukiwa umewasili Kijijini kwake Butibu Kata ya Kinamapula Halmashauri ya Ushetu Shinyanga kwa ajili ya wananchi wa wake kuanza kujiweka tayari kuanza taratibu za kuaga na baadaye kesho kuwekwa katika nyumba yake ya milele.  

Makamanda wa Jeshi la JWTZ wakitoa heshima kwa viongozi mbalimbali waliofika nyumbani kwa aliyekuwa Waziri wa Ulinzi Marehemu John Elias Kwandikwa kawa ajili ya kuanza taratibu za kuaga na baadaye kesho kupumzisha mwili huo katika Nyumba yake ya milele kijijini kwake Butibu Kata ya Kinamapula Halmashauri ya Ushetu Shinyanga.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com