METDO Tanzania

METDO Tanzania

Friday, October 9, 2020

KATIBU MKUU KUSAYA AWAPONGEZA CHAMA KIKUU CHA USHIRIKA CHATO KWA KUKUFUA KIWANDA CHA KUCHAKATA PAMBA

Mhe. Hussein Bashe Naibu Waziri Kilimo akihutubia Wanaushirika na Wananchi wa wilaya ya Chato walioshiriki kwenye hafla ya uzinduzi wa Chama Kikuu cha Ushirika Chato mchana leo mchana, tarehe 9 Oktoba, 2020.


Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya akihutubua Wakulima na Wageni walioshiriki kwenye hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha Chama Kikuu cha Ushirika cha Chato (Chato Cooperative Union – CCU Ltd) leo mchana, tarehe 9 Oktoba, 2020 wilayani Chato.


Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Robert Gabriel akihutubia Wanaushirika na Wananchi wa wilaya ya Chato walioshiriki kwenye hafla ya uzinduzi wa Chama Kikuu cha Ushirika Chato mchana leo mchana, tarehe 9 Oktoba, 2020.


Mkurugenzi Mkuu wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo (TADB) Bwana Justine Japhet akihutubia Wanaushirika na Wananchi wa wilaya ya Chato walioshiriki kwenye hafla ya uzinduzi wa Chama Kikuu cha Ushirika Chato mchana leo mchana, tarehe 9 Oktoba, 2020.


Wanachama wa Chama Kikuu cha Ushirika Chato wakicheza ngoma kusheherekea hafla ya uzinduzi wa kiwanda cha kuchakata pamba wilayani Chato, leo mchana, tarehe 9 0ktoba, 2020.

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya awapongeza Wanachama wa Chama Kikuu cha Ushirika wilaya ya Chato kwa kufufua kiwanda cha kuchakata pamba; Kiwanda kilichosimama kwa zaidi ya miaka 20.

“Nawapongeza kwa kuwa mmefufua kiwanda chenu na kwa kufanya hivyo, mmeunga mkono juhudi za Serikali ya Awamu ya Tano, inayoongozwa na Mhe. Dtk. John Joseph Pombe Magufuli ambapo amedhamilia kuifanya Tanzania iwe nchi ya tofauti.”

Huu ni mwanzo mzuri na Wanaushirika wa Chato hamjatuangusha, na hii ni ishara kuwa huko tuendako ni kuzuri”. Amekaririwa Katibu Mkuu Kusaya.

Aidha; Katibu Mkuu Kusaya ametoa pongezi kwa uongozi wa wilaya ya Chato, uongozi wa mkoa wa Geita kupitia Mkuu wa mkoa Mhandisi Robert Gabriel pamoja na uongozi wa Benki ya Maendeleo ya Kilimo inayoongozwa na Mkurugenzi Mkuu, Bwana Justine Japhet kwa kufanikisha mkopo wa zaidi ya shilingi bilioni 4 ambapo sehemu ya fedha hizo, ilitumika kukarabati mashine za kiwanda hicho.

Katibu Mkuu Kusaya ametoa wito kwa Wanachama wa Chama Kikuu cha Chato kuzalisha pamba zaidi ili uwepo wa kiwanda uwe na faida zaidi kuliko ilivyokuwa hapo kabla.

“Ndugu zangu Wakulima, tunawajibika kuongeza tija na uzalishaji wa pamba; Tumeambiwa uwezo wa mashine za kiwanda hiki ni kuchakata pamba kiasi cha kilo milioni 30 wakati ambapo uzalishaji wetu ni kilo milioni 8 hadi 12. Nataka niwahakikishie kuwa uwezo huo tunao, ni suala la maamuzi tu”.

“Nimeelezwa pia Wilaya ya Chato na Bihalamulo mnazalisha pamba safi na ya daraja la juu; Nitoe wito muanze kuzalisha kwa tija na mara dufu, uzalishaji uwe juu na si kilo 200 kwa eka za sasa, bali mzalishe kuanzia kilo 1,200. Uzalishaji huu unawezekana ikiwa mtatumia mbegu bora, mbolea, viuatilifu pamoja na Wataalam”.

“Jambo hili limewezekana kwa Wakulima wengine kwa nini kwenu lishindikane? Kwa msaada wa Wizara ya Kilimo, tutawasaidia kufika kwenye uzalishaji huo”. Amesisitiza Katibu Mkuu Kusaya.

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo ametumia nafasi hiyo kutoa agizo kwa Mkurugenzi wa Bodi ya Pamba kuhakikisha inasaidia kwenye kuongeza tija na uzalishaji kwa Wakulima wote nchini ili kutoa uzalishaji wa mwaka huu wa tani laki (120,000) ili uzalishaji urudi kama mwaka juzi; Tani laki (300,000) na hadi mwaka 2025 ufike tani laki (500,000).

Wakati huo huo Katibu Mkuu Kusaya amewakumbusha Wanachama wa Vyama vya Ushirika kote nchini kuendelea kutunza mali za Ushirika.

“Wanaushirika hizini mali zetu; Mnapaswa kuzitunza, zilipatikana kwa jasho kupitia Wazazi wenu na ninyi mnawajibika kuzitunza”. Amekaririwa Katibu mkuu.

Katibu Mkuu Kusaya ameongeza kuwa kila mali ya ushirika iliyochukuliwa isivyo hali, itarudishwa, zoezi la kurejesha mali za ushirika zilizoporwa lilianza mwaka 2016 kwa kusimamiwa na Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Majaliwa Kassim Majali na kwa litaendelea kuwa endelevu.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com