METDO Tanzania

METDO Tanzania

Wednesday, September 2, 2020

UPUNGUFU WA MIUNDOMBINU YA VYOO MASHULENI NA MAJI KARAGWE WORLD VISION YALETA SULUHISHO


 Shule za msingi za Biyungu na Kilruruma wilayani Karagwe Mkoani Kagera ni miongoni mwa shule zilizokuwa na changamoto kubwa ya vyoo vya wananfunzi kutokana na kuwa na idadi kubwa ya wananfunzi licha yakuwa shiri la World Vision kuasaidia katika sekta hiyo. 

Katika hafla ya kukabidhi matundu manane ya vyoo kwa kila shule yaliyojengwa na shirika lisilo la kiserikali la World Vision Tanzania Mradi wa Bushangaro AP kwa serikali ya mkoa,meneja wa shirika hilo kanda ya Kagera Juliana Charles amesema kuwa walifika katika shule hizo na kusikitishwa na hali waliyoikuta na kuwiwa kuanzisha ujenzi wa vyoo hivyo.

 

Juliana amesema kuwa shirika hilo linajihusisha Zaidi na makuzi ya mtoto hivyo kujenga miundombinu ya vyoo mashuleni ni moja ya huduma muhimu kwa mtoto ambayo itampelekea kusoma kwa raha lakini pia kuweza kumuepusha na magonjwa mbali mbali ya mlipuko yanayoweza kumtokea. 

 

Sambamba na ujenzi wa vyoo hivyo shirika hilo pia limekabidhi mradi wa maji ambayo mtandao wake umesambazwa kwenye vijiji viwili ambavyo vipo kata ya Bushangaro na kuweza kusambazwa katika zahanati ya Nyakagoyagoye ili kuweza kurahisisha huduma hiyo kwa jamii ya wanakaragwe.

 

Katibu Tawala wa mkoa Kagera Profesa Faust­ine Kamzora baada ya kukabidhiwa miradi hiyo ameitaka jamii kuitunza miradi na kutunza mazingira ili kuhakikisha ubora wa miradi unabaki ulele ule ambapo pia ameutaka uongozi utakaosiamamia mradi wa maji kuhakikisha maji hayo wanayatibu kabla ya kumfikia mwananchi ili kumuepusha na magonjwa.

 

Kamzora amesema mradi umejingwa kwa ufadhili wa nchi ya Ujerumani kwa garama ya zaidi ya shilingi milioni 400 na end­apo Mazingira ya mi­undomibun ya maji ya­kiwekwa kwenye hali ya usafi unao zingat­ia matunzo bora una­weza kuondoa magonjwa yanatokana na matu­mbo hasa kwa watoto wadogo.

 

Aidha Kamzora almesem­a,vituo vya afya na Hospitali na zahanati kwa asili­mia kubwa zinapokea matatizo ya magonjwa ya upungufu wa maji kwa asilimia 70 pamoja nna magonjwa ya tumbo kutokana na watu kutumia maji ambayo sio salama am­bayo yote hayo ni uk­osefu na uhaba wa ma­ji yenye uhakika .

 

“ pia maji yanafaida nyingi na sio kuond­oa magonjwa ya tumbo na upungufu wa maji mwili pekee bali na kuanzisha bustani majumbani na kujipat­ia lishe bora ya wat­oto lakini pia matumizi mengine ya nyumbani ikiwemo kufua na kufanyia usafi mwingine”amesema Kamzora.

 

Meneja wa shir­ika la Worldvision kanda ya Kagera Juli­ana Charles amesema mradi huo utahudumia wananchi ambao awa­li walikuwa wakitumia muda mrefu kufuata maji vijiji jirani ambayo bado yalikuwa hayapo katika usalama.

 

Charles amesema kuwa­,”baada ya kupatiwa taarifa na kamati ya maji kijijini hapo, shirika liliweza kufi­ka eneo la chanzo na kufanya tathimini ya shughuli ya ujenzi utakaoweza kuzua mif­ugo isiweze kuingia ndani ya maji hayo kwa kuyazumguzisha, .

 

Shirika limefanya ujenzi wa chanzo kwa kujengea maji ikiwa ni kuzuia mifugo,na kut­unza chanzo kisiweze kuharibiwa na jamii ambayo inatakiwa  yenywe itunze cha­zo hiki”.

 

Mwenyekiti wa kjiji cha Nyakagoyagoye Salmoni Mtilani alisema, kukamilika kwa ujenzi huo utao­ndoa watoto kutumia muda mwingi kutafuta maji na wakati mwin­gine kutokuhudhulia shuleni kwa ajiri wa­zazi wao kuwatuma maji umbari mrefu

 

“ Sio watoto sio waz­azi wao wanatembea umbari mrefu wa kilo­mita18 kwenda kijiji jirani kufuata maji ambayo hayachangam­ani na mifugo kijing­ine watoto kutohudhu­lia shuleni kabisa na kuwafanya kukosa masomo na hatimaye kushuka kitaaluma” Amesisitiza M­tilani

 

Mtilani alisema, kuwa kijiji cha Nyakag­oyagoye kilikuwa kina­fuata maji kijiji jirani kwa sababu cha­nzo ambacho kimefan­yiwa ujenzi wanajamii walikuwa wanayatum­ia kama maji ya mifu­go kwa mazinmgira yalikuwa hayalidhishi kwa wanajamii kwen­da kuchota maji hayo.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com