Wananchi wa Kitongoji cha Migombani,Kijiji cha Bukene, Wilaya ya
Nzega, Mkoani wa Tabora, wakimsikiliza Waziri wa Nishati, Dkt.Medard
Kalemani,(hayupo pichani) wakati wa uzinduzi wa mradi
Waziri wa Nishati, Dkt.Medard Kalemani
amezindua rasmi usambazaji wa Umeme katika kila kitongoji nchini ambapo jumla ya
vitongoji 64,839 nchini kote vinatarajiwa kuungalishwa na umeme kwa kipindi cha
miezi 12 kuanzia sasa.
Uzinduzi rasmi wa usambazaji umeme
katika kila Kitongoji umefanyika katika Kitongoji cha Ufuruma Kijiji cha
Ufuruma Wilayani Uyui na katika Kitongoji cha Migombani Kijiji cha Bukene
Wilayani Nzega mkoani Tabora, Septemba 24, 2020.
Dkt. Kalemani alisema kuwa mradi huo
utagharimu fedha za kitanzania shilingi Bilioni 297.7 na kwamba mradi huo ni
endelevu.
Akizungumzia sababu ya kuchagua Mkoa wa
Tabora kuwa kitovu cha kuzindua mradi huo, Dkt. Kalemani alisema kuwa mkoa huo
ni mkubwa ikilinganishwa na mikoa mingine nchini, pia una idadi kubwa ya
vitongoji ambavyo bado havijaunganishwa kabisa na umeme.
Katika mkoa huo, Vitongoji 122
vinatajiwa kuunganishiwa umeme na Kampuni ya Ukandarasi ya Sengerema ambayo
ndiyo imepewa dhamana ya kutekeleza kazi hiyo katika vijiji hivyo ambapo
ameahidi kutekeleza mradi huo ndani ya kipindi cha miezi Tisa, badala ya Miezi
12.
“Naomba tuelewane watanzania, Rais Magufuli na Serikali yake alikwisha toa fedha za kupeleka umeme kwenye vijiji vyote na vitongoji vyote,niwaombe watanzania kwenye masuala ya umeme tulieni umeme unakuja kila kitongoji bila kujali kwamba kimeguswa au laa, sasa ni rasmi kuwa vitongoji vyote vinaletewa umeme ,mnachotakiwa wananchi ni kusuka nyaya katika nyumba zenu na umeme huu haubagui nyumba,” alisisitiza Dkt. Kalemani.
Aidha aliendelea kuwataka wananchi kuendelea kulipia gharama za kuunganishiwa umeme bila kusubiri nguzo kuwafikia kwa kuwa tayari umeme utafika katika kila kitongoji kwa gharama ya shilingi 27,000 tu.
Vilevile alisema kuwa wananchi hawapaswi kuhoji kuhusu nguzo kufika katika maeneo yao kwakuwa hilo si jukumu lao, wanachotakiwa kufanya ni kulipia gharama za kuwashiwa umeme tu, na baada ya kulipia gharama ndipo wahoji endapo hawajawashiwa umeme.
Aliwata REA na TANESCO kushirikiana na serikali za vijiji, wilaya na mikoa kutoa elimu na kuwahamasisha wananchi juu ya umuhimu wa umeme na kuunganishwa.
Hata hivyo aliwaonya baadhi ya wakandarasi wenye tabia ya kuruka nyumba za wateja kuwa hiyo haitakubalika na yeyote atakaye binika kufanya hivyo hatua za kisheria itachukuliwa dhidi yake.
Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa huo,
Dkt. Philemon Sengati aliwaasa wananchi wa mkoa huo kuchangamkia fursa ya umeme
kwa kuanzisha viwanda vidogo ili kuinua uchumi wao na taifa kwa jumla.
Aidha amewataka kutunza miundombinu ya mradi huo na kutoa ushirikiano kwa wakandarasi wanaoetekeleza mradi huo na kwamba vijana watakaopata ajira wawe wazalendo na kuzingatia kuwa miradi hiyo ni kwa ajili ya watanzania.
0 comments:
Post a Comment