METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, August 9, 2020

WAZIRI HASUNGA AANZA ZIARA YA UKAGUZI WA MSIMU WA UNUNUZI WA PAMBA SIMIYU NA SHINYANGA

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga akizungumza na viongozi wa Chama cha Ushirika cha Ngolomamali kilichopo Wilayani Itilima leo Tarehe 9 Agosti 2020 wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku moja mkoani Simiyu kukagua msimu wa ununuzi wa Pamba mwaka 2020/2021. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga akizungumza na viongozi wa Chama cha Ushirika cha Maendeleo kilichopo Wilayani Itilima leo Tarehe 9 Agosti 2020 wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku moja mkoani Simiyu kukagua msimu wa ununuzi wa Pamba mwaka 2020/2021

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga akizungumza na viongozi wa Chama cha Ushirika cha Maendeleo kilichopo Wilayani Itilima leo Tarehe 9 Agosti 2020 wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku moja mkoani Simiyu kukagua msimu wa ununuzi wa Pamba mwaka 2020/2021

Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga akiwa katika picha ya pamoja na viongozi wa  Chama cha Ushirika cha Malita kilichopo Wilayani Maswa leo Tarehe 9 Agosti 2020 wakati akiwa kwenye ziara ya kikazi ya siku moja mkoani Simiyu kukagua msimu wa ununuzi wa Pamba mwaka 2020/2021

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Simiyu

Baada ya kumalizikia kwa Sherehe za Wakulima (NANENANE) Waziri wa Kilimo Japhet Hasunga leo Tarehe 9 Agosti 2020 ameanza ziara ya kikazi katika Mikoa ya Simiyu na Shinyanga ambapo pamoja na mambo mengine atakagua msimu wa ununuzi wa Pamba mwaka 2020/2021.

Ktiaka ziara hiyo Waziri Hasunga amemuagiza Mrajis wa Tume ya Maendeleo ya Ushirika Dkt Benson Ndiege kwa kusaidiana na Warajis wasaidizi wa Ushirika wa mikoa kuhakikisha kuwa wanatoa elimu ya kutosha kwa wanachama wa vyama vya Ushirika ili kuwa na elimu ya kutosha kuhusu usimamizi wa mali za ushirika, kadhalika umuhimu Ushrika.

Kutokana na Wakulima kulalamikia mfumo wa kuwalipa fedha wakulima wa Pamba kupitia kwenye Account za Benki, Waziri wa Kilimo amemuagiza Mrajis Msaidizi wa Vyama Vya Ushirika Mkoa wa Simiyu Ndg Ibrahim Kadudu kuzielekeza kampuni zinazonunua Pamba kuwalipa fedha taslimu wakulima wenye kiasi kidogo cha Pamba.

Agizo hilo limetokana na malalamiko ya viongozi wa vyama vya Ushirika alivyotembelea na kukagua msimu wa ununuzi wa Pamba ambavyo ni Maendeleo AMCOS na Ngolomamali AMCOS za Wilayani Itilima pamoja na Malita AMCOS kilichopo Wilayani Maswa.

Waziri Hasunga amesema kuwa Wizara yake imejipanga kufanya mazungumzo na Benki mbalimbali nchini pamoja na kampuni za simu ili kujadili uwezekano wa kupunguza bei za makato ya wakulima. “Dhamira yetu sisi kama serikali tunataka mkulima apate kiasi anachostahili kutokana na jasho lake makato makato sio sawa” Alisema

Pia, Waziri Hasunga amewataka wakulima wa Pamba nchini ambao hawajalipwa fedha zao kuwa wavumilivu wakati huu ambapo serikali inaendelea kulitafutia ufumbuzi jambo hilo ili kulitatua.

Katika Mkoa wa Simiyu wakulima wanadai Bilioni 2.9 ambapo tayari imeshawalipa wakulima kiasi cha takribani Bilioni 414.4 kati ya Bilioni 419 zilizokuwa zinadaiwa na wakulima wa Pamba kote nchini.

MWISHO

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com