METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, August 11, 2020

KATIBU MKUU KILIMO ATOA PIKIPIKI TATU/TREKTA DOGO KWA CHUO CHA MAFUNZO MATI MARUKU

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya akiongea na Wakufunzi na Wanachuo wa MATI Maruku mkoani Kagera leo tarehe 10 Agosti, 2020 kushoto kwake ni Mkurugenzi Idara ya Mafunzo na Utafiti na Huduma za Ugani Wizara ya Kilimo Dkt. Mashaka Mdangi

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya akiongea na Wakufunzi na Wanachuo wa MATI Maruku mkoani Kagera leo tarehe 10 Agosti, 2020 kulia kwake ni Mkuu wa Chuo cha MaATI Maruku Bwana Laurent Luhembe na mwengine Mkurugenzi Idara ya Maendeleo ya Mazao Wizara ya Kilimo Bwana Nyasebwa Chimangu

Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Bwana Gerald Kusaya akiongea na Wakufunzi na Wanachuo wa MATI Maruku mkoani Kagera leo tarehe 10 Agosti, 2020

Katibu Mkuu Kilimo Bwana Gerald Kusaya leo tarehe 10 Agosti, 2020 ametoa pikipiki tatu, trekta moja dogo aina ya ‘Power Tiller’ kwa ajili ya Wanachuo na Wakufunzi wa Chuo cha Kilimo Maruku (MATI Maruku) cha mkoani Kagera na kuahidi kuwanunulia basi (Coaster) ili kujibu changamoto ya Wanachuo ya usafiri, pamoja na mafunzo kwa vitendo (Field Practicum).

Katibu Mkuu Kusaya amesema, pikipiki hizo tatu zitakabidhiwa muda mfupi kuanzia wiki ijayo ili ziwasaidie Wakufunzi kutimiza majukumu yao kwa ufanisi.

Wakati huo huo Katibu Mkuu amesema Wizara ya Kilimo itatoa computer za mezani (Desktop Computers) pamoja na kufunga mfumo wa maktaba kwa njia ya mtandao (E – Library) pamoja na kufunga viyoyozi viwili (Sprit Units) kwa ajili ya chumba maalum cha ‘computer’ ya Wanachuo kujisomea.

“Napenda kuwafamamisha Uongozi wa Chuo cha MATI Maruku pamoja na Wanachuo; mahitaji yenu yote, Wizara imeyachukua na inafafanyia na itayatolea majibu haraka iwezekanavyo”.

“Mkuu wa Chuo andika mahitaji yote na yaje kwa maandishi, mahitaji ya kuboreshewa miundombinu ya maji pamoja na mfumo vya maji taka kwa vyoo vya mabweni ya Wanachuo wa Kiume, wiki ijayo nataka kuona Mkuu wa Chuo umewasilisha maombi haya ya miundombinu ya vyoo vya Wanaume ili ukarabai ukamilike kwa wakati, ndani ya mwezi huu wa Agosti”. Amekaririwa Katibu Mkuu.

Katibu Mkuu Kusaya pia ametoa kiasi cha shilingi milioni 10 kwa ajili ya kuanzisha mradi wa kisasa wa ufugaji wa kuku ambapo kiasi hicho cha fedha kitatumika kwa ujenzi wa banda la kisasa kufuga kuku kwa ajili.

Mradi huo utakisaidia Chuo cha MATI Maruku kama chanzo cha mapato kwa ajili ya kusaidia mahitaji mbambali ya Chuo pamoja na kutumika kama chanzo cha mapato pamoja na kujifunza dhana ya ujasiliamali.

Aidha Katibu Mkuu Kusaya ameahidi kutoa fedha kwa ajili ya kugharamia mafunzo ya nadharia na vitendo kwa Mkufunzi wa MATI Maruku (Bi. Esperance Anatory) ambaye ataenda kujifunza kuhusu ufugaji wa kuku walioboreshwa katika Kituo cha Mafunzo cha Silver land eneo la Ihemi, mkoani Iringa, muda mfupi ijao.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com