METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, July 25, 2020

RAIS MHE. DKT. MAGUFULI ASAINI KITABU CHA MAOMBOLEZO NA KUMPA POLE MJANE WA RAIS MSTAAFU WA AWAMU YA TATU MAREHEMU BENJAMIN MKAPA MAMA ANNA MKAPA NYUMBANI KWAKE MASAKI JIJINI DAR ES SALAAM



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli akisaini kitabu cha Maombolezo nyumbani kwa Marehemu Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa mara baada ya kuwasili nyumbani hapo wakati akitokea jijini Dodoma. 

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwa pamoja na wanafamilia wa Marehemu Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Benjamin William Mkapa wakimuombea sala Marehemu Mzee Mkapa nyumbani kwake Masaki jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimfariji Mjane wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Mzee Benjamin William Mkapa Mama Anna Mkapa nyumbani kwa Marehemu Masaki jijini Dar es Salaam. Kushoto ni Mke wa Rais Mama Janeth Magufuli

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akimfariji Mjane wa Rais Mstaafu wa Awamu ya Tatu Marehemu Mzee Benjamin William Mkapa Mama Anna Mkapa nyumbani kwa Marehemu Masaki jijini Dar es Salaam.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiwa pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli wakiwafariji na kuwapa pole familia ya Marehemu Mzee Benjamin William Mkapa nyumbani kwa Marehemu Masaki jijini Dar es Salaam.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli akiondoka msibani pamoja na Mkewe Mama Janeth Magufuli mara baada ya kutoa pole kwa familia ya Marehemu Mzee Benjamin William Mkapa nyumbani kwa Marehemu Masaki jijini Dar es Salaam. PICHA NA IKULU.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com