METDO Tanzania

METDO Tanzania

Saturday, June 6, 2020

TUNA USHIRIKIANO MZURI NA SERIKALI KWENYE UTEKELEZAJI WA HAKI ZA BIANADAMU-JAJI MSTAAFU MWAIMU


Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu (wa tatu kulia) akizungumza jambo katika kikao kifupi na Mkurugenzi wa Mashtaka wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibari, Ibrahim Mzee Ibrahim (wa kwanza kushoto), alipomtembelea ofisini kwake Mjini Unguja Zanzibari Juni 5, 2020, Kulia ni Kamishna Mkazi wa Haki za binadamu na Utawala bora  kwa upande wa Zanzibari, Khatibu Mwinyichande na Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo, Mohamedi Khamis Hamadi

Mkurugenzi wa Mashtaka wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibari, Ibrahim Mzee Ibrahim(wa kwanza kushoto)  akizungumza na ugeni wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora walipomtembelea  ofisini kwake Mjini Unguja, Zanzibari na kufanya kikao kifupi kuhusu masuala ya haki za binadamu, kulia ni  Mwenyekiti wa Tume hiyo, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu na Makamu Mwenyekiti, Mohamedi Khamis Hamadi.

Makamu Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu , Mohamedi Khamis Hamadi akifafanua jambo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka wa Serikali ya Mapinduzi,  ya Zanzibari ( hayupo pichani), kuhusu haki za binadamu walipomtembelea ofisini kwake Mjini Ungua, Zanzibari Juni 5, 2020., kulia ni Kamishna Mkazi wa Haki za binadamu na Utawala bora  kwa upande wa Zanzibari, Khatibu Mwinyichande na kushoto ni Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu

Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jaji Mstaafu.Mathew Mwaimu akizungumza na watendaji wa juu wa tume hiyo na Mkurugenzi wa Mashtaka wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibari, Ibrahim Mzee Ibrahim, wakati wa kikao kifupi kuhusu haki za binadamu kilichofanyika ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Mjini Unguja Zanzibari Juni 5, 2020.


Mwenyekiti wa Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu amesema kuwa ushirikiano baina ya Tume hiyo na Serikali ni Muhimu ili kutekeleza majukumu ya kuwapatia wananchi haki inayohitajika katika masuala mbalimbali ya jamii.

Akizungumza katika Ziara aliyoifanya Ofisi ya Mkurugenzi wa  Mashtaka iliyopo Mjini Unguja, Zanzibari Jaji Mwaimu alisema kuwa tume ya haki za binadamu ni chombo cha serikali ambacho kipo kisheri kwa ajili ya wananchi kikilenga ukuzaji na ulindaji wa haki  kwa pande zote mbili.

“Tume ni chombo cha Serikali ambacho kipo kisheria na majukumu yake ni kukuza na kulinda haki za binadamu na misingi ya utawala bora kwa Serikali na wananchi, tunafanya kazi ya kuisaidia Serikali maana yake pande zote mbili viongozi na wananchi kwa kushughulikia malalamiko  mbalimbali ya pande hizo”, Alisema Jaji Mwaimu.

Alisema kuwa lengo kuu la ziara ya kupita kila ofisi inayohusiana na masuala ya utekelezaji wa haki za binadamu ni kujenga mahusiano bora katika kitumiza azma ya kuiwezesha Serikali kujua mahali ambapo kuna ukiukwaji wa haki za binadamu ili iweze kutatua jambo hilo kwa haraka zaidi.

Naye, Mkurugenzi wa Mashtaka wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibari, Ibrahim Mzee Ibrahim alisema kuwa ataendelea kutoa ushirikiano kwa ofisi ya Tume hiyo kwa kuwa utekelezaji wa majuku yake unaendana na uwepo wa haki za binadamu.

“Majukumu ya ofisi yetu tunayoyafanya kila siku, mara nyingi yanahusiana sana na haki za binadamu kwa sababu mtu akikutwa na jinai yeyote moja kwa moja lazima haki yake iangaliwe na hukumu itolewa kwa kuzingatia sheria na haki za binadamu, kwa hiyo ushirikiano wetu na ofisi ya tume unahitajika sana na mimi nasema tutaendelea kutoa ushirikiano kwa ofisi yako”,  alisema  Ibrahim Mzee.

Aliongeza kuwa tume hiyo imepewa jukumu kubwa la kutekeleza na kuleta haki za binadamu, kwani imekuwa msaada mkubwa kwa Serikali na wananchi katika kulinda na kuweka hali sawa kwa malalamiko mbalimbali.

“Tume mumepewa jukumu zito, lakini naamini jukumu limefika kwenye mikono salama kwani mnakwenda vizuri na kasi ya Serikali ya Awamu ya Tano, na mumeleta heshima kwa tume hii na sasa inafanya kazi kwa manufaa makubwa ya wananchi na Serikali yao”, Alifafanua Ibrahim Mzee.

Kwa Upande wake Makamu Mwenyekiti wa Tume hiyo, Mohamedi Khamis Hamadi alisema kuwa tume imeendelea kushirikiana vizuri na ofisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka Zanzibari katika kuleta haki kwa wananchi na aliomba kuwepo na mashirikiano mbalimbali yakiwemo ya mafunzo kwa watumishi wa ofisi hizo mbili.

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com