METDO Tanzania

METDO Tanzania

Sunday, June 7, 2020

KAMPUNI YA QWIHAYA YAMPONGEZA RAIS MAGUFULI NA SHAMBA LA MITI SAO HILL KUTUNZA MAZINGIARA NA KUKUZA UCHUMI

 Meneja wa kampuni inayozalisha nguzo za umeme ya Qwihaya General Enterprise Co Ltd, Ntibwa Mjema  akiongea na waandishi wa habari katika kiwanda cha uzalishaji wa nguzo za umeme 
Mhasibu wa kampuni inayozalisha nguzo za umeme ya Qwihaya General Enterprise Co Ltd Abeid Mhongole akiongea na waandishi wa habari katika kiwanda cha uzalishaji wa nguzo za umeme 

NA FREDY MGUNDA,IRINGA.

KAMPUNI inayozalisha nguzo za umeme ya Qwihaya General Enterprise Co Ltd  imepongeza juhudi za kutunza mazingira zinazofanywa na shamba la miti la Sao Hill kwa kuendelea kutoa elimu ya upandaji wa miti na utunzaji wa mazingira kwa ujumla.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa Qwihaya, Ntibwa Mjema alisema kuwa kampuni hiyo inawapongeza na kuwashukuru wakala wa huduma za misitu Tanzania TFS kupitia shamba la miti la Sao hill Mkoani Iringa kuwa karibu na wadau wa misiti.

Mjema alisema kupitia shamba la miti la Sao Hill wamefanikiwa kutoa ajira kwa wafanyakazi zaidi ya mia mbili kupitia kiwanda hicho cha kuzalisha nguzo za Umeme ambazo kwa sasa zinasambazwa karibia nchi nzima.

Alisema shamba la miti Sao Hill limekuwa mfano kwa nchi nyingi Africa na nje ya Afrika kwa namna ambavyo linatumika katika kuhifadhi mazingira na kutoa ajira kwa watanzania wengi ambao wanapata faida kupitia shamba hilo.

Mjema alisema kuwa kupitia mazao msitu yanayopatikana katika shamba hilo la Sao Hill wamefanikiwa kuendeleza kukuza uchumi na maendeleo kwa ujumla kwa wananchi wengi hapa nchini na nje ya nchi.

Alisema kampuni inayozalisha nguzo za umeme ya Qwihaya General Enterprise Co Ltd inampongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kwa kuziamini kampuni za wazawa katika kufanya miradi mingi ya kimaendeleo ambayo sasa imeleta mabariko makubwa kwenye sekta mbalimbali

“Kamapuni ya Qwihaya ni kampuni ya kizalendo ambayo imeaminiwa kuzalisha nguzo za umeme ambazo zimekuwa zinasambazo nchi nzima hasa kwenye mradi wa REA ambao umekuwa unawanufaisha wananchi wengi wa kijijini ambao hapo awali walikuwa hawana umeme” alisema

Aidha Mjema aliwataka wakulima wa miti kuacha tabia ya kuvuna miti ikiwa bado michanga kwa kuwa soko lake linakuwa halina faida kwao na utunzaji wa mazingira kwa ujumla.

Kwa upande wake mhasibu wa kampuni ya Qwihaya Abeid Mhongole alisema kampuni hiyo imeajiri wafanyakazi zaidi ya mia mbili kutokana na mazao ya misitu ambayo yamekuwa yanatumika kutoka katika shamba la miti la Sao Hill.

Alisema kuwa shamba la Sao Hill limekuwa msaada mkubwa kwa kutoa ajira nyingi kwa watanzania na kusaidia kukuza uchumi kwenye sekta ya viwanda kutokana na mazao ya misitu ambayo yanapatikana katika shamba hilo.

Mhongole alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr John Pombe Magufuli kwa kazi kubwa anayoifanya kuleta maendeleo kwa watanzania hasa katika kuwaamini watanzania katika kuweka kwenye miradi mikubwa ya kimaendeleo.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com