METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, May 14, 2020

KATA YA KITWIRU BARABARA ZAKARABATIWA,WANANCHI WAPONGEZA

Diwani wa kata ya Kitwiru Baraka Kimata akiwa na burudoza likikarabati baadhi ya Barbara za mitaa ya kata ya Kitwiru

NA FREDY MGUNDA, IRINGA

Wananchi wa kata ya kitwiru wapongeza juhundi za diwani wa kata hiyo kwa kurekebisha miundombinu ya barabara ambayo itasaidia kukuza maendeleo ya wananchi.

Wakizungunza wakati wa ukarabati barabara za mitaa mbalimbali katika kata hiyo ya Kitwiru walisema jambo analolifanya diwani huyo ni kuhakikisha wananchi wanafanya shughuli za kimaendeleo bila ya vikwazo vyovyote vile.

Walisema kuwa mvua za msimu huu zimearibu barabara kwa asilimia kuwa na kupelekea kufifia kwa kazi za kimaendeleo kwa wananchi.

"Uwepo wa miundombinu bora ya barabara kunachangia kwa kiasi kikubwa shughuli za kimaendeleo kufanyika bila changamoto hiyo na kuleta maendeleo kwa kukuza uchumi wa wananchi "walisema 

Wananchi hao waliongeza kuwa wanachangamoto ya kukosekana kwa usafiri wa moja kwa moja wa kutoka Iringa mjini hadi Mitaa ya Nyamuhanga ambako asilimia kubwa ya wananchi wanaishi huko huku shughuli za kiuchumi wanazifanya Iringa mjini kwa asilimia kubwa.

Kwa upande wake diwani wa kata ya Kitwiru Baraka Kimata alisema kuwa jukumu kubwa ni kuwatumikia wananchi ili wafanye shughuli za kimaendeleo wakiwa hawana changamoto za miundombinu ya barabara.

Alisema kuwa huo ni mkakati endelevu wa uihakikisha wanaboresha miundombinu ya barabara kwenye mitaa yote ya kata ili kurahisiha shughuli za kimaendeleo za wananchi wote.

Kimata alisema kuwa juhudi za kukarabati miundombinu ya barabara inatokana na juhudi za kwake kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa manispaa ya Iringa mjini wanaopenda maendeleo ya wananchi wa kipato cha chini.

"Tumeanza ukarabati huu wa miundombinu ya barabara utakuwa endelevu kila uchwao ili kuhakikisha barabara zote za kata yangu ya Kitwiru zinapitika kirahisi na kurahisisha shughuli za kimaendeleo kwa wananchi" alisema kimata

Kimata alisema kuwa mvua za msimu huu ziliharibu miundombinu ya barabara kwa kiasi kikubwa na kukwamisha juhudi za maendeleo kwa wananchi wa kata ya KiKitwiru.

Kuhusu changamoto ya Usafiri wa dala dala na bajaji kutofika katika maeneo hayo Kimata alisema alikwisha zungumza na wamiliki wa magarinili waanzishe safari kupitia njia inayokatiza mitaa ya Nyamuhanga na kupatiwa kibari lakini changamoto iliyokuwapo awali ni hadi ya miundombinu chakavu hivyo ukarabati huo wa barabara utafungua fursa ya kuwapo kwa dala dala na bajaji zitakazoanza safari katika maeneo hao.

Kimata aliwahimiza wamiliki wa vyombo vya usafiri wa Umma kutumia fursa ya uhitaji wa usafiri katika maeneo hayo ili kujiongezea kipato na kuondosha kero ya usafiri kwa wananchi wa Nyamuhanga na kata ya Kitwiru kwa ujumla

Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com