METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, March 12, 2020

RC HAPI,ATOA SIKU TATU UONGOZI WA SOKO MAFINGA KUBORESHA HUDUMA YA CHOO

 Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akikagua miundombinu ya soko kuu la Mafinga wilaya ya Mufindi wakati wa ziara ya Iringa mpya awamu ya pili
  Mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi akikagua miundombinu ya soko kuu la Mafinga wilaya ya Mufindi wakati wa ziara ya Iringa mpya awamu ya pili akiwa na viongozi wa mkoa wa Iringa na wilaya ya Mufindi

NA FREDY MGUNDA,MAFINGA.
 
WAFANYABIASHA wa soko kuu la Mafinga mkoani Iringa wamelalamikia kukosekana kwa huduma bora ya choo kwa kuwa inahatarisha afya za wafanyabiashara hao.

Hayo yameibuka wakati wa ziara ya mkuu wa mkoa wa Iringa alipotembelea soko hilo kwa lengo la kukagua miundombinu na maendeleo ya wafanyabiasha wa soko hilo.

Baadhi ya wafanyabiashara wa soko hilo walisema kuwa wamekuwa wanachangia kiasi cha shilingi mia kila anapokwenda kupata huduma hiyo,lakini choo hiyo inahari mbaya ya kimiundombinu kiasi cha kusababisha magonjwa kwa watumiaji wa huduma hiyo ya choo.

Akijibia hoja mkuu wa mkoa wa Iringa Ally Hapi aliutaka uongozi wa soko kuu la Mafinga kutumia siku tatu kuhakikisha wanatatua tatizo la huduma ya choo ambayo imekuwa kero kwa wafanyabiashara wa soko hilo.

Alisema kuwa wafanyabiashara wanalipia fedha kupata huduma hiyo ya choo lakini mazingira sio salama kulinga na thamani ya ambayo inatolewa na watumiaji wa huduma hiyo.

“Haiwezekaji kila mwezi mnapokea zaidi ya shilingi laki tisa lakini mnashindwa kuboresha huduma kwa wanyabiashara wa soko hivyo natoa siku tatu tu kuhakikisha wanaboresha huduma hiyo la sivyo ataufuta uongozi huo” alisema Hapi

Hapi alisema kuwa uongozi unatakiwa kujenga choo kipya na bora ili kuboresha huduma ya choo,kwa kuwa kila mfanyabiasha hulipa kiasi cha shilingi mia moja  na tayari wameshalipa kiasi cha shilingi elfu kumi na zinatosha kabisa kuboresha huduma hiyo.

Aidha Hapi alimtaka mkurugenzi na uongozi wa soko kuhakikisha wanatatua tatizo la takataka,choo na vibanda vya kufanyia biashara kwa kuwa vimekuwa kero kwa wafanyabiasha wa soko hilo.

Kwa upande wake mkurugenzi wa halmashauri ya Mji wa Mafinga Sada Mwaruka alisema kuwa watahakikisha wanatatua kero hizo kwa lengo la kuhakikisha wanaboresha huduma ya soko kuu hilo la mafinga.
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com