Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya
Mkuu wa Kitengo cha Teknolojia za unyunyiziaji viuatilifu(TPRI) Mhandisi Julius Mkenda (Kulia)akitoa maelezo kwa Katibu mkuu Wizara ya Kilimo Gerald Kusaya ya matumizi ya mabomba na vinyunyizi.
Katibu Mkuu wizara ya Kilimo Ndg Gerald Kusaya akikagua mangala ya kuhifadhia nafaka ya Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula wakati akiwa katika ziara ya kikazi Jijini Arusha.
Na Innocent Natai, TPRI-Arusha
Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Gerald Kusaya amekasirishwa na kitendo
cha baadhi ya watendaji wa Wizara hiyo
kukaimu nafasi za watu kwa zaidi ya miezi sita bila sababu ya msingi suala
linalowafanya washindwe kutekeleza majukumu yao kwa uhuru,Ufanisi mkubwa na kuweka
malengo na mikakati yenye manufaa zaidi.
Kusaya ameyasema hayo katika ziara yake ya kuzitembelea taasisi
zilizopo chini ya Wizara ya Kilimo Mkoani Arusha,(Taasisi
ya Utafiti wa Viuatilifu vya Kudhibiti Visumbufu katika Ukanda wa Kitropiki (TPRI), Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) na Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ( CPB ) ziara yenye lengo la kufahamiana
na watumishi na kupata taarifa za utendaji kazi wa Taasisi hizo.
Akizungumzia changamoto hiyo amesema kwa kipindi kifupi tangu awepo Wizara
ya Kilimo ameshuhudia baadhi ya watendaji wa Wizara hiyo wakiendelea kuitwa
makaimu kwa muda mrefu bila sababu ya msingi.
“Jana kwenye baraza la wafanyakazi niliwaambia hili suala na leo nasema,mtu awekaimu kwa sababu ya kukaimu kwa muda mfupi eidha kwasababu mkuu wa taasisi ametoka na isizidi miezi sita na aikizidi huko kutakuwa sio kukaimu”Alisema
Kusaya.
Aidha ameeongeza kuwa endapo anayekaimu anayosifa ya kuwa kwenye ile nafasi
haitaji kuwa kwenye ile nafasi kwa muda mrefu aangaliwe kwa muda mfupi na
endapo ataonekana anayosifa za kuwa kwenye nafasi ile basi apewe ile nafasi ili
aendelee na majukumu yake na endapo anayekaimu hana sifa basi atafutwe mwenye
sifa na kupewa ile nafasi.Ikiwa ni ili kuwaondolea hofu watendaji na kuwafanya
wafanye maamuzi kwa kujiamini na waweze kuweka mipango madhubuti ya kuleta
maendeleo.
Aidha Kusaya ameridhishwa na kazi
zinazofanywa na Taasisi hizo ikiwemo ya TPRI na kuwataka kuongeza juhudi za
kufanya tafiti mbalimbali za visumbufu vya mazao na mimea ili kuhakikisha
wanawasaidia wakulima kujikwamua kiuchumi.
Pia amewataka wataalamu na wakaguzi kutoka Taasisi hiyo ya TPRI kuhakikisha
wanatokomeza viuatilifu visivyo na ubora vinavyoingizwa hapa nchini kwa njia za panya,Sambamba na hilo ameahidi kushirikiana bega kwa bega na TPRI
kuhakikisha wanaokutwa wanauza au kusambaza viuatilifu vilivyoisha muda wa
matumizi,Visivyo na ubora(Bandia) wanapata adhabu itakayowafanya wajute kufanya
biashara hizo.
Aidha pia Kusaya amewataka watendaji wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA)
kanda ya Arusha kuzidi kutekeleza
majukumu yao vyema ili kuhakikisha taifa linakuwa na hifadhi yakutosha ya
chakula ili panapotokea changamoto ya uhaba wa chakula serikali iwezekutatua changamoto
hiyo.
Aidha ameipongeza Bodi
ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko ( CPB )kutokana na jitihada watendaji wake
wanazozionyesha za kuhakikisha wakulima wa Mikoa ya Kanda ya
Kaskazini kuondokana na adha ya masoko ya kuuzia mazao yao hususani mahindi ili
kutumia wanayoyatumia katika kiwanda cha CPB kilichoanza uzalishaji hivi karibuni.
CPB ambayo zamani ilijulikana kama
‘Monaban’ imekuwa ikinunua mazao ya wakulima wa kanda ya Kaskazini na kuzalisha
bidhaa mpya ya unga wa dona ijulikanayo kwa jina la ‘Dona bora’ unga unaopendwa
ambapo pia utasaidia serikali kuongeza pato kupitia biashara wanazozifanya.
Ziara ya Katibu Mkuu Wizara ya Kilimo, Gerald
Kusaya inatarajiwa kuendelea kwa siku moja zaidi mkoani Arusha na baadae
kwa siku moja Mkoani Kilimanjaro ambapo mkoani hapo atatembelea Bodi ya Kahawa
0 comments:
Post a Comment