METDO Tanzania

METDO Tanzania

Tuesday, December 10, 2019

MHANDISI MTIGUMWE AAGIZA BODI NA WATENDAJI WA SACCOS KUWASILISHA RASIMU ZA TAARIFA ZA FEDHA KWA WAKAGUZI WA NJE COASCO KABLA YA JANUARI 31, 2020


Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe

Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dodoma

Katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo Mhandisi Mathew Mtigumwe ameiagiza Bodi na Watendaji wa SACCOS kuwasilisha Rasimu za Taarifa za Fedha kwa Wakaguzi wa Nje (COASCO) kabla au ifikapo tarehe 31.01.2020.

MHandisi Mtigumwe ametoa agizo hilo Jijini Dodoma ambapo amesema kuwa ni lazima kuwasilisha mapema taarifa hizo ili Ukaguzi uweze kufanyika kwa wakati na Taarifa za Ukaguzi ziwasilishwe kwa Mamlaka husika ndani ya muda uliopangwa Kisheria.

Amewataka wanachama wote wa SACCOS hususani Bodi na Watendaji wa SACCOS nchini kuwa, matakwa ya Sheria ya Huduma Ndogo za Fedha ya Mwaka 2018 (The Microfinance Act 2018), kuhusu ukaguzi wa nje hivyo ni lazima kutekeleza agizo hilo kwa wakati.

“SACCOS zote zinatakiwa kuhakikisha kuwa Taarifa za Fedha za Mwaka 2019 ziwe zimekaguliwa na kuwasilishwa Benki Kuu au kwa Mamlaka iliyokasimiwa ambayo ni Mrajis wa Vyama Vya Ushirika ifikapo tarehe 30 Aprili, 2020” Alisema

MWISHO
Share:

1 comment:

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com