METDO Tanzania

METDO Tanzania

Thursday, November 21, 2019

SHAKA:VIONGOZI WA UPINZANI NI WACHANGA KISIASA VYAMA VYAO VINATEGEMEA SERA YA ULALAMISHI


Na mwandishi wetu, Morogoro

Chama cha Mapinduzi (CCM) mkoa Morogoro kimesema kitendo cha baadhi ya vyama vya upinzani kususia uchaguzi wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji utakaofanyika Novemba 24 mwaka huu vimeonyesha jinsi vilivyo na uteke wa fikra kisiasa na kukosa kujiamini.


Ikiwa aina ya viongozi walionao wataendelea na siasa za kususia uchaguzi, kusubiria kupinga matokeo kama alivyozoea aliyekuwa mgombea urais wa CUF Maalim Seif Sharif Hamad vitasubiria kwa miaka mingi ijayo kushika dola. 


Matamshi hayo yametamkwa jana na katibu wa CCM Mkoa wa Morogoro Shaka Hamdu Shaka wakati akitoa tathimini ya CCM mkoa huo kuelekea uchaguzi ambapo kati ya vijiji 669 CCM imepita 664, mitaa 327 CCM imepita 325 na vitongoji 3,358 CCM imepita 3,320 huku vyama vya CUF, Chadema, UDP act wazalendo vikiendelea kusimamisha wagombea katika vijiji 5, mitaa 2 na vitongoji 38.


Shaka alisema kususia uchaguzi hakutoi majawabu yakinifu kutokana na malalamiko ya upinzani badala yake vyama hivyo vilipaswa kushiriki kisha vilalamike huku wakiwa na ushahidi kama zilikuwepo dosari, itikadi au mapungufu kadhaa lakini kususia tu wakati hawana jambo la kuwaonyesha wananchi badala yake wanabaki kulalamika kama vifaranga vya kuku ni kuonyesha uteke wa maarifa ya kisiasa na udhaifu mkubwa kwa upinzani nchini. 
“Wapinzani wa Tanzania wakubali wasikubali bado wateke kisiasa. 


Viongozi wao wepesi na dhaifu mno kiupeo na kiufahamu. Hawajengi nguvu za hoja bali ni walalamishi .


 Kama wagombea wenu wamekiuka kanuni za uchaguzi jawabu si kususa ifikie wakatiupinzani usitafute huruma huo ni uzembe na kwa vyovyote vile sasa wabadilike na waache utoto wa kisiasa.”Alisema Shaka


Amefahamisha kuwa upinzani hauwezi kujilinganisha na ukomavu wa viongozi wa CCM kisiasa kwani uchanga wa wa vyama vyao na ikiwa vitaendelea na siasa za kupiga mayowe bila kuwa na hoja za maana vyama hivyo vitaendelea kukosa mipango na oganaizesheni ya kisiasa mwisho vitapoteza muelekeo na kupotea katika ramani za kisiasa.


“Vinaonekana kwenye maeneo ya mijini wakipiga kelele mitaani.Hawapo kwenye vitongoji wala vijijini kwasababu haviungwi mkono. Hata wagombea wao mijini wana jazba na kujikuta wakishindwa hata kujaza fomu kwa mujibu taratibu na kanuni alafu etibaada ya kujimarisha kutokana na mapungufu yao wanaendelea kujichimbia kaburi” Alieleza Shaka


Akitoa mfano alikitaja chama cha ACT Wazalendo ambacho alidai hakikuwahi kuwa hata na wanachama visiwani Zanzibar, nacho sasa kimeanza kujigamba kuwa kitashinda urais mwaka 2020 kwakuamini tu Maalim seif aliyehama CUF atakipa ushindi Chama hicho. 


Hata hivyo Shaka alimtaka kiongozi mkuu wa chama hicho Zitto kabwe kufuta ndoto za kupata ushindi Tanzania bara wala Zanzibar kwa kuzingatia kuwa siasa za Zanzibar ni nzito na atambue kuwa hata Maalim Seif Sharif Hamadi zilimshinda tokea akiwaCCM na baadae CUF kisha kuamua kuhamia ACT Wazalendo ambako nako hataweza na hatamudu kubadili hata koma kwenye sentensi.


“Wagomee kushiriki uchaguzi lakini waache kabisa kuchochea ghasia na fujo. Msingi mkuu wa Serikali za CCM ni kulinda amani, umoja na utulivu hivyo atakayethubutu kuanzisha fujo dola haitamuacha azidi kugharimu maisha ya wasio na hatia, nawaomba wananchi wote wajitokeze kwa wingi 24 Novemba kutimiza haki yao ya kikatiba kuwachagua viongozi wao wa mitaa, vijiji na vitongoji” Alieleza Shaka 


Source Mtanzania, Uhuru, Majira, la Jiji
Share:

0 comments:

Post a Comment

Copyright © WAZO HURU | Powered by Blogger Design by ronangelo | Blogger Theme by NewBloggerThemes.com